Ijumaa, 14 Oktoba 2016

NAIBU WAZIRI TAMISEMI SULEIMAN JAFO AMEWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA WAADILIFU

Posted by Esta Malibiche on Oct14.2016 in NEWS

f3
Naibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa, Selemani Jafo, akiongea na watumishi wa Halmashauri wa Babati.

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amekemea tabia iliyokuwa ikifanywa awali na baadhi wa watumishi wasio waadilifu kwa kuchukua rushwa kwa wakandarasi wa miradi ya ujenzi kwa kuwalazimisha kutoa fedha ili kupewa kazi na kuidhinishiwa malipo yao.
Jafo alisema kwamba kumekuwa na tabia ya “Utatu usio mtakatifu ” katika halmashauri ambo una athiri sana utekelezaji wa miradi ya ujenzi.
Utatu huo unawahusisha Afisa Manunuzi, Mhandisi wa ujenzi, na mweka Hazina (DT), ambapo Jafo alisema kwamba halmashauri ikiwa na kazi ya ujenzi Afisa Manunuzi anaweza mazingira kupata fedha ili mkandarasi apewe kazi.
Mkandarasi akishapata kazi anakutana na kizingiti kingine kutoka kwa Mhandisi (Engineer) ambaye anagoma kupitisha certificate yeyote ya kazi iliyofanyika mpaka apewe chake mapema.
 Kizingiti cha tatu kinajitokeza pale Mweka Hazina  (DT) kugoma kuandaa malipo na kutoa cheki ya mkandarasi hadi apewe chake. Haki hii  inamfanya Mkandarasi wa ujenzi anajikuta ametoa fedha nyingi ili apate kazi na kupokea malipo.
 Kutokana na Utatu huo, umesababisha baadhi ya miradi kujengwa chini ya kiwango hivyo kuharibika baada ya kipindi kifupi.
Jafo alikemea tabia hiyo alipokuwa akikagua miradi ya maendele na kuongea na watumishi wa halmashauri za wilaya ya Babati, Mbulu, Nzega, Igunga na Iramba.
Aliwataka wafanyakazi wa halmashauri kufanya kazi kwa kujiamini na kuzingatia kanuni za utumishi wa umma.
Aliwaagiza wakurugenzi kukuza vipaji vya watendaji wao kwani wengi wao japo ni wasomi wazuri lakini wamekuwa hawatumiki vyema na baadhi yao kutopewa kipaumbele katika idara zao.
f1
Naibu Waziri wan chi, Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa, Selemani Jafo, akiongea na kina mama wajawazito wanaosubiria kujifungua katika jengo maalum kwa kinamama wanaotoka mbali ili kuepuka vifo vya kinamama wakati wa kujifungua katika hospitali ya Iramba, Singida.
f2
Naibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa, Selemani Jafo,akikagua hospitali ya wilaya ya Iramba mkoani Singida.

f4

0 maoni:

Chapisha Maoni