Jumapili, 23 Oktoba 2016

MAN UNITED YA MOURINHO YABUGIZWA VIKOMBE VINNE NA CHELSEA LIGI KUU YA UINGEREZA.


Posted by Esta Malibiche on Oct 23.2016 in MICHEZO

imagesTimu ya Chelsea imeibuka na ushindi wa kishindo wa mabao 4-0 kwa kuwafunga Man United ya Kocha Jose Mourinho ambaye alitimuliwa mwaka jana na Chelsea hivyo leo ilikuwa mara ya kwanza kukanyanga uwanja wa Stamford Bridge mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza na hiki ndicho kipigo kikubwa msimu huu kukipata mashetani hao.

Pedro alikuwa wa kwanza kuipatia goli timu yake dakika ya mapema ya pili kwa pasi ya Marcos Alonso baada ya kufungwa Man United walikuwa juu huku wakiwa wakitumia style ya kushambulia na kujilinda na dakika ya 21 walifungwa goli la pili likifungwa na beki kisiki Gary Cahill kwa kichwa hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele.

Kipindi cha pili kilianza kwa Chelsea kuendelea kulishambulia lango la Man United,licha ya mashetani hao kumiliki mpira kwa asilimia kubwa walijikuta wakifungwa goli la tatu kupitia kwa winga hatari Eden Hazard dakika ya 62 kuingia kwa goli hilo liliwachanganya vijana wa Mourinho na katika dk ya 70 kiungo aliyesajiliwa kutoka kwa Leicester City N’golo Kante alifunga goli la nne huku likiwa la kwanza kwake msimu huu.

Chelsea wakitumia mfumo wa mabeki watano nyuma uliwapa wakati mgumu Man United na kujikuta wakizidiwa kila idara ya mchezo na kucheza mpira wa ovyo na kujichanganya na kushindwa kujua namba fulani anacheza nani na kwa matokeo hayo Chelsea wanapanda hadi na nafasi ya nne wakiwa na pointi 19 wakati Man United wameshuka hadi nafasi ya mtaa wa saba yaani ya saba kwenye msimamo.

0 maoni:

Chapisha Maoni