Katika kuhakikisha magonjwa yatokanayo na Pneumococcal yanatoweka duniani, waalamu wa afya kutoka nchi mbalimbali Afrika na watengenezaji wa chanjo inayotumika kukinga watoto na magonjwa mbalimbali kama Nimonia wamekutana katika mkutano wa siku tatu wa Kanda ya Afrika uliyo na malengo ya kujadili magonjwa yanayotokana na Pneumococcal.
Magonjwa ambayo yanatona na Pneumococcal ni pamoja na Nimonia (homa ya mapafu), homa ya uti wa mgongo na maambukizi ya damu ambapo wataalamu hao na watengenezaji wa damu kwa pamoja watajadili jinsi gani wanaweza kutokomeza magonjwa hayo katika nchi zao.
Akizungumza na MO BLOG, Meneja wa Taifa wa Mpango wa Chango kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dafrossa Lyimo amesema mkutano huo utaweza kusaidia kuona ni jinsi gani wataweza kutokomeza kabisa magonjwa yanayotokana na Pneumococcal na zaidi ugonjwa wa Nimonia licha ya takwimu kuonyesha kuwa kwasasa Tanzania inafanya vizuri.
Meneja wa Taifa wa Mpango wa Chango, Dafrossa Lyimo Meneja wa Taifa wa Mpango wa Chango kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dafrossa Lyimo akizungumza kuhusu mkutano huo na kutoa takwimu za Tanzania.
Amesema pamoja na mafanikio ambayo wameyapata lakini bado wanataka kuhakikisha wanaondoa kabisa uwezekano wa ugonjwa huo kuwapata watoto ambao wamekuwa wakipatiwa chanjo tangu wawapo watoto wachanga.
“Tumekuwa tukipokea chanjo kutoka shirika la GAVI ambazo tumekuwa tukigawa nchi nzima ili kila mtoto aweze kupata, sisi tunachukua chanjo Milioni 1.9 kwa mwaka na takwimu zetu zinaonyesha watoto 97% wamekuwa wakipata chanjo na kwasasa tunajiuliza jinsi gani tutakamilisha ifike 100,
“Changamoto ambayo inajitokeza ni wazazi wengine kutokupeleka watoto wakapate chanjo, wengine wanawapa mara moja au mbili na hii chanjo mtoto anatakiwa kuipata mara tatu, wiki ya sita tangu azaliwe, wiki ya kumi na wiki ya 14,” alisema Dafrossa.
dsc_0270Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Pfizer, Heather Sings akielezea sababu ya kuandaa mkutano huo na malengo ambayo watayaweka baada ya mkutano.
Aidha aliwataka wazazi kuwa wakiwapeleka watoto katika chanjo kwani madhara ambayo yanaweza kujitokeza ni makubwa na ambayo yanaweza kusababisha wakasimama kufanya shughuli za kiuchumi kwa ajili ya maisha yao na kuanza kuhangaika kupata matibabu ambayo kama wangezingatia mapema wangeweza kujiepusha na hilo.
Tanzania ilianza kutoa chanjo ya PVC13 ya kujikinga na Nemonia kwa watoto kutoka Shirika la GAVI tangu Januari, 2013 na GAVI inataraji kusitisha kutoa msaada huo mwaka 2025 hivyo nchi za 18 za Afrika ambazo zinapokea msaada huo zimetakiwa kuanza kujiandaa kwa ajili ya kujinunulia dawa pindi misaada ya chanjo hiyo itakapomalizika.
dsc_0244Mkurugenzi wa Sayansi wa Shirika la AMP, Dk. Bradford Gessner akielezea moja ya mada ambayo wanazijadili katika mkutano huo wa siku tatu.
dsc_0248Baadhi ya watu waliohudhuria mkutano huo kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika.
dsc_0245
dsc_0247
dsc_0255