Jumamosi, 8 Oktoba 2016

MBUNGE WA MKULANGA ABDALAH ULEGA AZINDUA KISIMA CHA KISASA KATIKA SHULE YA MSINGI LUPONDO

Posted by Esta Malibiche on Oct8.2016 in NEWS

Mbunge wa Mkuranga,Mhe. Abdallah Ulega,kupitia  Chama cha Mapinduzi(CCM)Mbunge wa Mkuranga,  akikata utepe wa uzinduzi wa kisima  cha maji katika Shule ya Msingi Lupondo,iliyopo kijiji   cha Lupondo  kilichojengwa na kwa ufadhiri wa shirika la  African Reflection Foundation. 

Akizungumza Mara baada ya kuzindua Kisima hicho, amesema kuwa kijiji cha Lupondo kilikuwa na changamoto ya maji kwa muda mrefu. Amesema kuwa wananchi hao walikuwa wakitafuta maji umbali wa kilomita tano na kufanya kuumiza kichwa katika kuwapata wafadhili wa mradi huo. 

Mhe.Abdallah Ulega amesema katika kipindi cha miezi tisa ameweza kupata miradi ya maji katika vijiji sita na kuahidi kuendelea kutafuta miradi ya maji katika vijiji vilivyosalia.Hata hivyo katika uzinduzi huo Mh.Ulega ametoa msaada wa mifuko 10 ya saruji katika msikiti wa kijiji hicho. 

Nae mratibu wa African Reflection foundation, Shiraz Mohamed, amesema wataendelea kufadhili miradi ya maji katika vijiji vyenye changamoto hiyo. 

.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa kijiji cha Lupondo jana mkoa wa Pwani
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lupondo kabla ya uzinduzi wa kisima cha maji katika kijiji cha Lupondo jana mkoa wa Pwani.

0 maoni:

Chapisha Maoni