Alhamisi, 13 Oktoba 2016

WAMILIKI WA SHULE BINAFSI WALIA NA RIBA KUBWA ZA KIBENKI

Posted by Esta Malibiche on Oct13.2016 in NEWS





Na Esta Malibiche
Iringa
WAMILIKI wa shule binafsi na vyuo ukanda wa nyanda za juu kusini Nyasa (TAMONGSCO) wameamua kuunda saccos yao  itakayowasaidia  kuendesha shule na vyuo vyao kutokana na taasisi za kuwapa fedha kwa riba kubwa jambo linalowafanya kujiendesha kwa hasara.
 Wakizungumza na kwenye mkutano wa drarura wa kupitisha katiba ya saccos hiyo  mwenyekiti wa Tamongsco mikoa ya Iringa,Njombe na Ruvuma Lucas Mwakabungu alisema ili kuondokana na changamoto hiyo wameamua kuanzisha saccos yao  itayowasaidia  kukopa fedha za kuendesha shule na vyuo pale wanapokwama.
“Ndugu wanachama saccos yetu hii ndioyo itakuwa mkombozi wetu kwani kila mmoja wetu hapa anajua adha na karaha ya tasisi za fedha pindi unapoenda kukopa fedha wanakuwa na masharti magumu na wakati mwingine kucheleweshewa hela uliyoomba  lakni kwa umoja wetu huu kila mmoja atakuwa ni mmiliki wa saccoso hii na utapata mkopo kwa wakati muuafaka ’’
  Mwakabungu alisema kuwa kwa kuwa benki zinatoza riba kubwa  na upatikanaji wa mikopo inachukua muda mrefu  ndiyo maana wameamua  kuanzisha saccos  ambayo itawakomboa kwa kiasi kikubwa na wanategemea ndani ya miezi sita wawe na zaidi ya Mil.500.
 Naye katibu wa tomongsco kanda ya nyasa Nguvu Chengula ambaye ni mmiliki wa shule ya Sun Academy alisema kuwa shule nyingi zinapofikia mwishoni mwa mwaka zinakumbwa na uhaba mkubwa wa rasilimali fedha kwa ajili ya kuendesha shule zao na ndio maana wameanzisha saccos hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwao na riba nafuu tofauti na benki.

Chengula alisema kuwa tasaisi nyingi za fedha ziwemekuwa zikiwapa masharti magumu yakutaka mtu kuwekeza vitu vya garama zikiwemo nyumba au gari ili hali muhusika hana vitu kwa kuwa ndio mchanga katika kuaendesha taasisi za elimu

“Kuna kipindi unaweza kuwa umekwama na huna fedha za kuendeshea shule na shuleni unawanafunzi wanahitaji chakula na vitu vingine unaenda kwenye taasisi za fedha lakini unazungushwa wewe mpaka kuja kupata hiyo fedha na matatizo tayari yamewikisha sasa huo mkopo unatakuwa na maana gani”
 Kwa uapande wake Noah Mtokoma ambaye ni mwenyekiti wa saccos hiyo ya ukanda wa nyasa alisema kuwa uaminifu,uadilifu ndicho kitu cha muhimu ambacho kitafanya saccos hiyo kukuwa kwa haraka

0 maoni:

Chapisha Maoni