Jumanne, 11 Oktoba 2016

MGANGA MKUU WA SERIKALI PROF. MUHAMMAD BAKARI AZINDUA MRADI WA JENGO LA UPASUAJI NA KITUO CHA DAMU SALAMA MKOANI IRINGA

Posted by Esta Malibiche On Oct12.2016 in KITAIFA





 Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Muhammad Bakari  ambae ni Mgeni Rasmi akimwakilisha Waziri wa Afya,katika uzinduzi wa miradi ya maendeleo iliyofanyika mkoani Iringa.Pembeni yake ni Katibu tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu



Na Esta Malibiche
Iringa

MGANGA Mkuu  wa Serikali Prof. Muhammad Bakari amewataka watumishi  na Afya Nchini kuendelea kuwaudumia wananchi kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao  ili wagonjwa wanaofika  Hospitalini waweze kupata matibabu yaliyo bora.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya  katika uzinduzi wa mradi wa jengo la upasuaji na kituo cha kutolea damu katika Hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa,iliyojengwa kwa ufadhiri wa Hospital ya Vicenza kutoka  Italia pamoja nakampuni ya Asas iliyoko mkoani Iringa,Prof.Muhamad alisema kuwa  njia bora ya kulipa fadhira kwa wafadhiri waliojitolea kujenga ni kuhakikisha wananchi wanapata  huduma bora zaidi na stahiki  ili kuwatia moyo wahisani  na hatimae kuendelea kutoa  misaada mingi na mikubwa zaidi.
‘’’’’’’Sera ya Serikali  ni kuhakikisha inashirikiana kwa ukaribu na wadau mbali mbali wa maendeleo zikiwemo Taasisi na Mashirika ya  kidini na Taasisi na mashirika ya Kimataifa, katika kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini. Hivyo napenda kuchukua nafasi hii kuupongeza sana Uongozi wa Mkoa wa Iringa kwa jitihada walizofanya ili kulifanikisha jambo hili la ushirikishwaji wa wadau. Haya tunayoyashuhudia leo hii yasingewezekana kamwe kama hali ingekuwa vinginevyo. Hivyo naomba kuwatia moyo muendelee na jitihada hizi za kushirikisha wadau na wananchi kwa ujumla katika utatuzi wa changamoto za kiafya zilizopo.’’’’’’’’alisema Prof.Muhamad
Prof.Muhamad alisema kuwa,  miongoni mwa Malengo endelevu ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inapunguza vifo vya akina mama wakati wa uzazi na vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano. Pia malengo hayo, yametafsiriwa na kueendana sambamba na Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi, (MMAM]
.
‘’’’’’’Natambua kuwa tunazo changamoto nyingi katika kufikia malengo yetu, ikiwa ni pamoja na kutokuwa na wataalamu wa kutosha na wa fani zote muhimu katika utoaji wa huduma za Afya. Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa watumishi waliopo kazini ni asilimia 51tu ya mahitaji yote ya watumishi wa sekta ya Afya. Upungufu huu umeathiri zaidi taaluma nyeti, ikiwemo taaluma ya huduma kwa wagonjwa mahututi (ICU) na wale wa nusu kaputi (Anaesthesiologists). Ili kutatua changamoto hii, Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kufundisha na kuajiri wataalam wa Afya, hasa wa fani zenye upungufu mkubwa, na vile vile kutoa kipaumbele cha kuwapeleka Watumishi wanaojiriwa katika maeneo yenye upungufu mkubwa zaidi, ili kuboresha huduma kulingana na uwezo wa bajeti. Aidha, kwa vile mchakato wa ajira za Watumishi unaanzia katika Halmashauri na Mikoa kwa kuweka mahitaji hayo katika bajeti, hususani ya hospitali, napenda niwasisitizie kuwa wakati wa upangaji wa bajeti mzingatie mahitaji yenu ikiwa ni pamoja na wataalamu wa huduma za wagonjwa mahututi na nusu kaputi’’’’’’Alisema Prof.Muhamad
‘’’’’Kama mnavyofahamu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) hupanga wataalamu kulingana na mahitaji na idadi ya nafasi tunazopewa. Hivi sasa mnatambua kuwa ajira zimesitishwa, hivyo pindi ruhusa ya kuajiri itakapotolewa mtapatiwa hao wataalamu kadri itakavyokubalika..Kwa wataalam wetu nawapongeza kwa kufanya kazi kwa kujituma, hata katika uchache wenu, na katika mazingira yenye mapungufu mengi. Nitoe rai tena kuwa muendelee kuwahudumia wananchi kwa moyo wote, na kwa kuzingatia maadili na weledi wa Taaluma zenu’’’’’’’Alisema Prof.Mahamud
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt.Robert Salimu akisoma taarifa ya miradi hiyo alisema, kuwa miradi hiyo itasaidia kuboresha utoaji wa huduma  za upasuaji mdogo na mkubwa kutokana  na eneo kubwa la kufanyia kazi,Kuzuia magonjwa ya kuambukiza kati ya wagonjwa,Kupunguza vifo vinavyotokana na upasuaji,Kupunguza gharama za Rufaa, kufuata huduma za kibingwa Hospitali ya Muhimbili na Hospitali za Kanda,Kuongeza nafasi kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu wa Tiba kujifunza pamoja na Kuwavutia madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa na Kanda kuja kufanya upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa

Dkt Robert aliongeza kuwa moja ya changamoto inayoikabili Hospitali hiyo nipamoja na kutokuwepo kwa wataalamu wa kutoa dawa ya usingizi (Anaethetist) katika Hospitali  hiyo,hivyo aliiomba Serikali iweze kusaidia kutatua changamoto hiyo.
Awali Mganga  mkuu mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt.Maseleta Nyakiroto  akisoma  taarifa ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa alisema kuwa ,Hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto ni uchakavu wa gari la kubebea wagonjwa [Ambulance] inayopelekea kuharibika mara kwa mara na kusababishia gharama kubwa za matengenezo  na kuleta usumbufu kwa wagonjwa pindi wapatapo refaa.
‘’’’’Hospitali hii inakabiliwa na uhaba wa watumishi hasa madaktari bingwa,Maafisa wauguzi,na wataalamu wengine.Pia idara ambazo hazina madaktari bingwa hivi sasa zinasimamiwa na madaktari wa kawaida,hali  hii inaathiri utoaji wa huduma  bora kwa wagonjwa’’’’’ alisema Nyakiroto
Nyakiroto alisema kuwa changamoto nyingine inayowakabili  ni ufinyu wa bajeti inayotengwa kwa matumizi ya kawaida[OC] na kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba kupitia MSD.Kutosekana kwa baadhi ya dawa muhimu na vifaa tiba mara kwa mara bohari ya dawa ya kanda
‘’’’’’Mheshimiwa Waziri tunakabiliwa na uhaba wa nyumba za watumishi hasa madaktari na madaktari bingwa.Pia tuna ukosefu wa wa kitengo muhimu kama vile kitengo cha kuhudumia  wagonjwa mahututi [ICU] na kitengo cha huduma ya dharura [Casualty/Emegency Unit]’’’’alisema Nyakiroto
MWISHO

 Askofu wa jimbo katoliki la Iringa Tarcisius Ngalalekumtwa ambae ni Rais wa Baraza la Maaskofu katoliki Tanzania kushoto kwake ni Mganga mkuu wa  mkoa wa Iringa Robert Salim
 

 
 Watumishi wa Afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa wakisikiliza kwa makini

  Watumishi wa Afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa wakisikiliza kwa makini
  Mganga Mkuu mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa Dkt.Museleta  Nyakiroto akisoma Taarifa ya Hspital ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa



 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt.Robert Salim akisoma Taarifa ya Miradi ya M,aendeleo iliyozinduliwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Ahammad Bakari
 

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu akizungumza 

 Mganga Mkuu wa Seriokali Prof.Muhammad Bakari akitoa Hotuba yake katika,katika uzinduzi huo
 

 Mganga Mkuu wa Seriokali Prof.Muhammad Bakari akiendelea kuzungumza


Mganga Mkuu wa Serikali Pro.Muhammad Bakari akizindua jengo la upasuaji lilijengwa kwa ufadhiri wa Hospitali ya Vicenza kutoka Itali

Mganga Mkuu wa Serikali Pro.Muhammad Bakari akiwa katika picha ya pamoja na katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu ,Mganga mkuu kutoka Hospitali ya Vicenza nchini Itali Pamoa  na baba  Askofu wa Jimbo Katoliki  la Iringa Tarcisius Ngalalekumtwa mara baada ya kuzindua jengo la upasuaji lililojengwa chini ya usimamizi wa Mhashamu baba Askofu
 

Mganga Mkuu wa Serikali Muhamad Bakari akikagua chumba cha upasuaji
 
 Mganga Mkuu wa Serikali Muhamad Bakari akikagua na kupokea maelezo katika chumba cha upasuaji
 
 

 Mhashamu baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa Tarcisius Ngalalekumtwa ambae pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzazia akishangiliwa na watumishi wa Hospitali hiyo na kupongezwa kwa kuleta wafadhiri waliojitolea katika ujenzi wa jengo hilo

Mganga Mkuu wa Serikali Pro.Muhammad Bakari,Katibu Tawala wa Mkoa wa Irina Wamoja Ayubyu Pamoja na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Robert Salim wakielekea katika jengo la kuchangia damu salama


 Mganga Mkuu wa Serikali Pro.Muhammad Bakari,akisalimiana na Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa Joseph Lyata ambae pia ni Diwani wa kata ya Kwakilosa kupitia chama cha Democrasia na Maendeleo [CHADEMA]

 


Mganga mkuu wa Serikali Prof.Muhmmad Bakari akisalimiana na wafanyakazi katika kituo cha damu salama kilichojengwa na Kampuni ya Assas

 Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Muhammad Bakari akizindua kituo cha Damu salama kilichojengwa na Kampuni ya Assas



 Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Muhammad akikagua  kituo cha Damu salama kilichojengwa na Kampuni ya Asas baa ya uzinduzi.Picha na Esta Malibiche[ KALI YA HABARI BLOG]






















0 maoni:

Chapisha Maoni