Jumatano, 19 Oktoba 2016

MRADI WA PELUM TANZANIA WAFANYA MDAHALO WA KUTOA ELIMU YA HAKI MILIKI YA ARDHI KATIKA VIJIJI VITANO WILAYANI KILOLO

 Posted by Esta Malibiche on Oct 19.2016 in NEWS
Meneja wa  shirika la Pelum Tanzania  Rehema Fidelis akitoa  maelezo kuhusu shirika  na mradi kwa wananchi  ][hawapo pichani]wa wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa wakati wa mdahalo  ulioandaliwa na shirika la PELUM uliofanyika wilayani Kilolo ukiwahusisha wananchi wa Wilaya ya Kilolo na Iringa Dc
Na Esta Malibiche 
Kilolo
WAKAZI wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wameishauri Serikali kusimamia sheria ya ardhi ili kukabiliana na migogoro ya ardhi inayotokea kwenye maeneo mbalimbali ya vijijini kama nia mojawapo ya kuimarisha uamani na utulivu na kuifanya sekta hiyo ya ardhi kuwa na tija kwa jamii.

Akizungumza kwenye  mdahalo wa siku moja uliofanyika jana Wilayani Kilolo Mkoani hapa Charles Mkiwa aliituhumu serikali za vijiji kuwa chanzo cha migogoro kutopkana na tabia ya baadhi ya viongozi kushindw akusimamia sheria pindi wanapotoa maamuzi yahusuyo masirahi ya ardhi kwenye maeneo yao.

“Migogoro hii imekuwa ichangiwa hasa na serikali za vijiji ambazo kwa nyakati tofauti zimetoa maamuzi ya matumizi ya aardhi bila kufuata sheriaa ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi ili kupata ushauri na sheria zinavyoelekeza”alisema Mkoga na kuongeza:

“Ikiwa sheria hizi zitazingatiwa ninaamini hakuna migogoro itakayoendelea kujitokeza ,lakini pia nitumia fursa hii kushuruku shirika la Pelum Tanzania kwa kwa kutekeleza mradi wa mradi wa ushiriki wa wananchi katika sekta ya kilimo kwa kwua umesaidia kuinua uelewa wa masuala ya ardhi miongoni mwa wananchi”alisema.

Kwa upande wake Bahati Mkove aliomba serikali kutenga maeneo baina ya wakulima na wafugaji  waliopo vijijini na kwamba kwa kufanya hivyo kutasaidia makundi hjaya kuepukana na migogoro kwa kuwa makundi yote mawili yanategemeana.

Meneja miradi wa Shirika la Pelum Tanzania ambalo  ndio walioandaa mdahalo huo Rehema Fedelisi alisema shirika lake limeamua kufanya kazi hiyo kwa lengo la kusaidia kukuza uelewa wa wananchi juu ya ya haki zao kwa masuala yahusuyo ardhi na mbinu za kukabiliana nayo ili kupunbguza tatizo hilo nchini.

Alisema kwa sasa mradi huo unatekelezwa katiak vijiji 30 vilivyopo katika wilaya sita za mikoa mitatu ya Tanzania bara na kwamba tangu utekelezaji huo umeanza mwaka 2013 watu wengi wameelimika na kuanza kutanmbua haki zao na kutatua migogoro inayohusu maeneo yao.

Akiwasilisha mada katika mdahalo huo afisa mradi wa Pelum Tanzania Angolile Rayson alisema utafiti uliofanywa na shirika hilo mwaka 2014 katika wilaya ya Kilolo ulibaini kuwa migogoro ya ardhi ya kwa wananchi wanaogombea mipaka katika maeneo ya vijijini ni asilimia 61 ya migogoro yote.

Alisema katika kuhakikisha wananchi wanakabiliana na changamoto hiyo shirika lake limetoa elimu na kuimarisha kamati za ardhi za vijiji,mabaraza ya ardhi ya vijiji ili yaweze kutatua migogoro pindi inapojitokeza kwenye maeneo yao.

Awali akifungua mdahalo huo katibu tawala wa Wilaya ya Kilolo Yusuph Msawanga aliwataka washiriki wa madahalo huo kutumia fursa hiyo kutoa changamoto zilizopo katika sekta ya ardhi kama njia ya kuzitafutia ufumbuzi.

“Migogoro mingi ya ardhi imekuwa ikitokea kuanzia ngazi ya familia,jamii kijiji kwa kijiji na hata wilaya kwa wilaya…shirika hili licha ya kutupatia elimu bado leo limetukusanya kwa lengo la kutupatia elimu”alisema Msawanga na kuongeza:

“Nitoe wito kwa washiriki wote mtoa mawazo yenu hapa ili mwisho wa siku yaweze kufanyiwa kazi jambo litakalosaidia kuondoa migogoro ya ardhi katika maeneo yetu na kutuletea maendeleo ya kiuchumi na ustwai wa kijamii”alisema.

 


 Washiriki wa mdahalo wakiendelea kusikiliza mada mbalimbali zinazowasilishwa


 Mdahalo ukiendelea



 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilolo Yusuph Msawangaakifungua Mdahalo huo, aliwataka washiriki  kutumia fursa hiyo kutoa changamoto zilizopo katika sekta ya ardhi kama njia ya kuzitafutia ufumbuzi



 Akiwasilisha mada katika mdahalo huo Afisa mradi wa Pelum Tanzania Angolile Rayson alisema utafiti uliofanywa na shirika hilo mwaka 2014 katika wilaya ya Kilolo ulibaini kuwa migogoro ya ardhi ya kwa wananchi wanaogombea mipaka katika maeneo ya vijijini ni asilimia 61 ya migogoro yote.




Washiriki wa mdahalo wakiendelea na majadiliano,ambapo Joseph Peter alisema kuwa ili Migogolo ya ardhi iweze kumalizika  ardhi inayomilikiwa na wananchi  inatakiwa kupimwa na kupewa hati miliki za kimira kwa mtu mmoja mmoja.w

 Katika kuchangia kwake Mjadala Rashid Abdalah alisema  sheria na taratibu za umiliki ardhi zinatakiwa kufuatwa pamoja na usimamizi wa utekelezaji wa wajibu wa Ardhi.Pia alisema kuondokana na migogoro ya ardhi miongoni mwa watumiaji wa ardhi vijijini Elimu ya umiliki Ardhi inatakiwa kutolewa kwa wananchi.





Wananchiwakiendelea  kuchangia mawazo katika ,kutokana na mada iliyosema nini kifanyike kuhakikisha Migogoro ya ardhi inaisha
 Mada mbalimbali zonazohudu haki ya umiliki ardhi zikiendelea kutolewa na muwezeshaji   ambae pia ni Mratibu wa shirika la Pelum
  Kwa upande wake Bahati Mkove aliiomba serikali kutenga maeneo baina ya wakulima na wafugaji  waliopo vijijin.Pia alisema kuwa  ni vema Halmashauri na viongozi wa kijiji wakashirikiana kwa pamoja wakati wa kupima ardhi na kumilikisha maeneo ili kuepusha na Migogoro kutokea



0 maoni:

Chapisha Maoni