Postedy by Esta Malibiche on August 16.2016 in News
Afisa Tawala Wilaya ya Tabora mjini Mhe. Sweetbert Nkuba, (kushoto)
akipokea moja ya madawati 90 yaliyotolewa na Dr.Amon Mkoga Foundation
na kukabidhiwa kwake na mwenyekiti wa Taasisi hiyo Ndugu.Amon
Mkoga(kulia). Anayeshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Sarah Kibonde Msika ambao ni wadhamini wa kampeni hiyo iitwayo “Simama Kaa”
Mwenyekiti wa Taasisi ya Dr.Amon Mkoga
Foundation Ndugu.Amon Mkoga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya
wanafunzi wa shule ya Isike Manispaa ya Tabora.
Mwenyekiti wa
Taasisi ya Dr.Amon Mkoga Foundation Ndugu.Amon Mkoga akiwa katika picha
ya pamoja na wanafunzi wa shule ya Isike kulia ni Amina Rajabu na
kushoto ni na James Shija.
…………………………………………………………………………
Taasisi ya Dr.Amon Mkoga
Foundation imetoa msaada wa madawati 90 yenye thamani ya shilingi
milioni 5.5 kwa shule za msingi katika manispaa ya Tabora, ikiwa ni
mchango wa Taasisi hiyo katika kuisaidia serikali kukabiliana na
upungufu wa madawati katika shule za msingi nchini.
Akizungumza leo katika hafla ya
makabidhiano iliyofanyika katika ofisi ya mkuu wa wilaya Tabora mjini ,
Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Ndugu Amon Mkoga amesema mchango huo ni
sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya taasisi hiyo ya kuunga mkono
jitihada mbalimbali za kuleta maendeleo nchini.
“Mchango huu ni sehemu ya
jitihada mbalimbali zinazofanywa na Dr.Amon Mkoga Foundation katika
kusaidia utekelezaji wa miradi yenye tija kubwa kwa jamii. Tunaamini
kwamba kupitia msaada huu, Taasisi yetu inatoa mchango wake katika
kujenga viongozi wa baadaye wa taifa hili na wanataluuma mbalimbali
wakiwamo madaktari, wahandisi na wengineo, “amesema Mkoga.
Makabidhiano yalihudhuriwa na Afisa Tawala Wilaya ya Tabora mjini Mhe. Sweetbert Nkuba
ambaye alisema madawati hayo 90 yataboresha mazingira ya kujifunzia kwa
watoto katika Mkoa wa Tabora na kutoa wito kwa wadau wengine kuunga
mkono zoezi hilo.
0 maoni:
Chapisha Maoni