Jumamosi, 20 Agosti 2016

SOPHIA MJEMA: ILALA YAKAMATA WANAFUNZI HEWA 599 KATIKA SHULE 6

1
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Ilala wakati alipotangaza kupatikana kwa wanafunzi hewa 599 katika shule 6 za wilaya hiyo ambapo uchunguzi wa wanafunzi wengine hewa bado unaendelea.
2
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akisisitiza jambo wakati alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Ilala wakati alipotangaza kupatikana kwa wanafunzi hewa 599 katika shule 6 za wilaya hiyo, Kulia ni Mkurugenzi wa Wilaya hiyo Bw. Edward Mpogolo.
3
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema  akifafanua jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Ilala wakati alipotangaza kupatikana kwa wanafunzi hewa 599 katika shule 6 za wilaya hiyo.
…………………………………………………………………………………………………..
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema ametangaza kupatikana kwa wanafunzi hewa 599 katika shule 6 za wilaya ya Ilala ambazo hakuzitaja, Mjema amesema baada uchunguzi huo kumegundulika wanafunzi idadi hiyo ya  ambapo wahusika wote watachukuliwa hatua za kinidhamu lakini pia sheria itachukua mkondo wake kwani hayo ni makosa kama yalivyo makosa mengine
Wilaya ya Ilala ina shule za sekondari za serikali 46 na za sekondari 49 ukiacha shule za taasisi binafsi ,zoezi la ukaguzi bado linaendelea katika shule zote za msingi wilayani humompaka Septemba 1 mwaka huu ndiyo litamalizika.
Akizungumzia suala la Madawati  mkuu wa wilaya huyo amewapongeza wadau wote waliochangia madawati mpaka kuhakikisha  uhaba wa  madawati katika wilaya ya Ilala unakwisha huku kukiwa ziada  ya madawati 2821 
Ameongeza kuwa kazi kubwa inayofuatia kwa sasa ni kuongeza vyumba vya madarasa ambapo kazi hiyo inaendelea vizuri .
Mh. Sophia mjema pia amemshukuru Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa kuanzisha mkakati  wa wadau kuchangia madawati jambo ambalo limesaidia tatizo hilo kushughulikiwa kikamilifu na wadau mbalimbali,  lakini pia akampongeza Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda kwa usimiamizi thabiti wa utekelezaji wa mkakati huo jambo ambalo limesaidia wilaya ya Ilala kumaliza kabisa tatizo la uhaba wa  madawati katika shule za zake za msingi

0 maoni:

Chapisha Maoni