Jumamosi, 27 Agosti 2016

Vijana nchini watakiwa kujijengea tabia ya kupenda kujifunza.

Postedy by Esta Malibiche on August 27.2016 in News

HT1
Meneja wa Buni Hub Jumanne Mtambalike akifafanua jambo katika Majadiliano yaliyoratibiwa na Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) kwa lengo la kujadili Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni muongoza mada Amon Tamilwai. Jukwa hilo limekuwa likikutana kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo ukutanisha vijana kwa lengo la kujadili mada mbalimbali zenye muelekeo wa kumkomboa kijana kifikra.
HT2
Mratibu wa Program kutoka Actuality Media Bi. Audrey Fancher akielezea jambo katika Majadiliano yaliyoratibiwa na Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) kwa lengo la kujadili Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Jukwa hilo limekuwa likikutana kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo ukutanisha vijana kwa lengo la kujadili mada mbalimbali zenye muelekeo wa kumkomboa kijana kifikra.
HT3
Baadhi ya Vijana wakichangia mada katika Majadiliano yaliyoratibiwa na Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) kwa lengo la kujadili Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Jukwa hilo limekuwa likikutana kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo ukutanisha vijana kwa lengo la kujadili mada mbalimbali zenye muelekeo wa kumkomboa kijana kifikra.
HT4
Baadhi ya washiriki wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) wakifuatilia mada katika Majadiliano kuhusu Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Jukwa hilo limekuwa likikutana kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo ukutanisha vijana kwa lengo la kujadili mada mbalimbali zenye muelekeo wa kumkomboa kijana kifikra.
HT5
Baadhi ya washiriki wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) wakibadilishana mawazo mara baada ya kumaliza Majadiliano kuhusu Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Majadiliano hayo yameratibiwa na Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).
HT6
Baadhi ya washiriki wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) wakibadilishana mawazo mara baada ya kumaliza Majadiliano kuhusu Ripoti ya Hali ya Ajira kwa Vijana ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Kazi Dunia (ILO) jana Jijini Dar es Salaam. Majadiliano hayo yameratibiwa na Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).
HT7
HT8 HT9
Baadhi ya waratibu wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF), kutoka kulia ni  Mkurugenzi Mkuu wa wa TASEF Adian Nzamba, Mratibu wa TASEF Bi. Genoveva Emanuel Mtiti na  Mshereheshaji Amon Tamilwai.
…………………………………………………………………….
Na: Frank Shija, MAELEZO.
Vijana nchini wanatakiwa kujijengea mazoea ya kupenda kujifunza kila wakati ili kuendelea kuibua mawazo endelevu kwa mustakabari wa maendeleo yao.
Hayo yamesemwa na Rais wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) Adrian Nzamba wakati wa majadiriano ya Ripoti ya Hali ya Ajira iliyoandaliwa naShirika la Kazi la Dunia (ILO) wakati wa majadiliano yaliyoandaliwa na Jukwaa hilo jana  Jijini Dar es Salaam.
“Vijana tunatakiwa tuwe na moyo wa kujifunza, wengi wetu wamekuwa wazito kujifunza” . Alisema Adrian.
Aliongeza kuwa kupitia Jukwaa hilo wamekuwa wakiwajengea uwezo Vijana katika hatua ya kujitambua na kuepukana na mawazo mgando yenye fikra hasi.
Kwa upande wake Meneja wa Buni Hub mshiriki mwenza wa Jukwaa hilo Jumanne Mtambalike ameipongeza Serikali kwa mchango wake katika kusaidia Vijana kufikia malengo yao.
Mtambalike amesema kuwa wao kama Buni Hub wamekuwa chini ya Tume ya Sayansi Tanzania (COSTECH) ambayo ni Taasisi ya Serikali hivyo ni dhahiri kuwa Vijana wakijitambua wanazo fursa nyingi kupitia Serikali yao kwani wao kama taasisi binafsi lakini wananufaika.
Aliongeza kuwa lengo kubwa la kushiriki Jukwa hilo ni kuwajengeauwezo vijana wa kufikiri na kujitegemea badala kukaa na kulalamika bila sababu ya msingi.
“Vijana tumekuwa na tabia ya kulalamika sana, zipo fursa nyingi tu ili mradi unapata taarifa tafuteni taarifa zipo fursa nyingi sana binafsi nilipata udhamini wa kusoma nje ya nchi kupitia Wizara ya Habari kwa sababu nilitafuta taarifa”. Alisema Mtambalike.
Aidha alitoa rai kwa Taasisi za Elimu ya Juu kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuangaliana namna ya kuwa na njia bora ya kuwaandaa vijana ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira.
Katika Jukwaa hilo vijana waliibua hoja mbalimbali zikiwemo kubadilisha mfumo  wa Elimu ili kuingiza mitaala ya Ujasiriamali, vijanga kujishughulisha na utafutaji wa taarifa na msisitizo wa vijana kushiriki katika kazi za kujitolea.

0 maoni:

Chapisha Maoni