Alhamisi, 25 Agosti 2016

KATIBU MKUU WA MALIASILI NA UTALII, MAJ. GEN. GAUDENCE MILANZI AMEWATAKA MAJANGILI WATAFUTE KAZI NYINGINE

ru1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akifunga mafunzo maalum ya kupambana  na ujangili kwa Askari wanyamapori katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida jana. Mafunzo hayo yatawasaidia Askari wanyamapori kupata taarifa za kitenteligensia kwa ustadi wa hali ya juu katika kupambana na kukabiliana na  majangili. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru2
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childress akizungumza wakati wa kufunga mafunzo maalumu ya ya kupambana  na ujangili kwa Askari wanyamapori katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida jana. Mafunzo hayo yatawasaidia Askari wanyamapori kupata taarifa za kitenteligensia kwa ustadi wa hali ya juu katika kupambana na kukabiliana na  majangili. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru3
Askari wanyamapori wakionesha kwa vitendo wakati wa kuhitimu mafunzo maalumu  yaliyofanyika katika Pori la Akiba la Rungwa  Mkoani Singida yaliyohitimishwa jana wakionesha namna ya kupambana na majangili  wakati  wakiwakamata majangili ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru4
Askari wanyamapori wakionesha kwa vitendo wakati wa kuhitimu mafunzo maalumu  yaliyofanyika katika Pori la Akiba la Rungwa  Mkoani Singida yaliyohitimishwa jana wakionesha namna ya kupambana na majangili  wakati  wakiwakamata majangili ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru5
Baadhi ya askari wanyamapori waliohitimu mafunzo wakiwa kwenye paredi jana katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida,  Mafunzo hayo yatawasaidia Askari wanyamapori kupata taarifa za kitenteligensia kwa ustadi wa hali ya juu katika kupambana na kukabiliana na  majangili. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru6
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania ( TAWA) Childress akizungumza wakati wa kufunga mafunzo maalumu ya ya kupambana  na ujangili kwa Askari wanyamapori katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida jana. Mafunzo hayo yatawasaidia Askari wanyamapori kupata taarifa za kitenteligensia kwa ustadi wa hali ya juu katika kupambana na kukabiliana na  majangili. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
ru7
Askari wanyamapori wakionesha kwa vitendo wakati wa kuhitimu mafunzo maalumu  yaliyofanyika katika Pori la Akiba la Rungwa  Mkoani Singida yaliyohitimishwa jana wakionesha namna ya kupambana na majangili  wakati  wakimkama ta jangili akiwa amejisalimisha yeye mwenyewe. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
…………………………………………………………………………
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi   ametoa  wito kwa  watu wanaojihusisha na vitendo vya ujangili waache kazi hiyo  baadala yake watafute kazi nyingine zitakazoweza kuwaingizia vipato halali kwa  kufanya hivyo wataweza kujiepusha kutiwa nguvuni na askari wanyamapori waliobobea kwa kazi hiyo.
Milanzi alitoa wito huo  jana    wakati wa  akifunga  mafunzo maalumu ya kupambana na Ujangili kwa askari wanyamapori  katika pori la akiba la Rungwa mkoani Singida yaliyofadhiliwa na Marekani na yaliyotolewa na Kikosi maalum cha wanajeshi kutoka Marekani.
Amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa askari wanyamapori  ili kuendelea na kukabiliana na wimbi kubwa la ujangili kwa kuwa majangili wasasa wanatumia silaha za kisasa tofauti na majangili wa  zamani ambao walikuwa wakitumia upinde na mishale.
Aliongeza kuwa majangili  wa sasa ambao askari wanyamapori wamekuwa wakikabiliana nao maporini  ni wale ambao  wanatumia silaha za kivita  hiyo ni lazima askari wetu  wapewe mafunzo ya hali ya juu ili waweze kukabiliana nao.
Aidha Katibu Mkuu, Milanzi alisema Wizara imejipanga kuhakikisha suala la ujangili linakwisha ambapo kituo  kingine cha mafunzo ya kijeshi kwa askari wanyamapori cha Mlele kilichopo Mkoani Katavi kimeanzishwa mbali na  vyuo vya  Pasiansi na Mweka, Likuyu Sekamaganga ambavyo pekee ndivyo vilivyokuwa vikitoa mafunzo kwa askari wanyamapori.
Aliongeza kuwa,  kwa sasa Serikali imejipanga kwa kushirikiana na Interpol  kuhakikisha kuwa hatakamatwa jangili tu aliyehusika  kuua mnyama porini bali mtandao wote utakamatwa na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria mahali popote.
Akizungumza na wahitimu wa mafunzo hayo, Milanzi alisema mafunzo hayo yamejikita kuwasaidia kupambana na majangili, magaidi pamoja na majambazi ambapo wao ndo watu wa kwanza kukumbana nao wakiwa porini kwani ndiko wanakotumia kujificha  kwahiyo ujuzi walioupata umewaongezea ufanisi katika kulinda maliasili zilizopo kwenye maeneo yao.
Aliwataka pia wahitimu hao kufanya kazi kwa kujituma wasiishie tu kusherekea kumaliza mafunzo bali waonyeshe kwa vitendo hii itasaidia na kuipa ari Marekani pamoja na  Asasi za kimataifa zenye lengo la kusaidia nchi katika vita dhidi ya Ujangili.
Kwa upande wake  Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childress amewataka wahitimu wazingatie mafunzo waliyopata kwa kuyafanyia kazi ili Pori la Akiba la Rungwa liwe sehemu salama kwa wanyamapori wanaopatikana katika pori hilo.
Ameahidi kuwa nchi yake itaendelea kuisaidia  Tanzania kwa kuwa suala la ujangili bado ni kubwa linalohitaji ushirikiano wa pande zote ili liweze kutokomezwa.

0 maoni:

Chapisha Maoni