Alhamisi, 25 Agosti 2016

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA MJUMBE WA KAMATI KUU CHADEMA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU EDWARD LOWASA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI, MBEYA,SONGWE,NJOME NA IRINGA

Postedy by Esta Malibiche on August 25.2016 in SIASA with no Comment













Mjumbe wa kamati kuu na waziri mstaafu Edward Lowasa  akiendendelea na vikao vya ndani mkoani mbeya,uliofanyika mbeya vijijini,tarehe 22 .2016 mkoa wa Songwe eneo la Vwawa na Tunduma ikiwa na lengo la kkijenga chama katika operation ya UKUTA september 1



































Mh.Lowasa akiendelea na mikutano ya ndani ya chama cha Democrasia na Maendeleo mkoani Njombe tarehe 23.8.2016
















Ilula


Iringa Mjini


Mjumbe wa kamati kuu na waziri mstaafu Edward Lowasa  akiendendelea na vikao vya ndani mkoani IRINGA tarehe 25.8.2016,akiwa mkoani Iringa alitembelea kata Ilula na baadae kuhitimisha katika jimbo la Iringa mjini  ikiwa na lengo la kukijenga chama katika maandalizi ya operation UKUTA september 1


Ilula


Mbunge wa viti maalum chadema Mh.Risala Kabongo akiwa na diwani wa kata ya Ilula chadema Raymond Francis mara baada ya kumalizika kikao cha ndani Ilula

WAZIRI Mkuu  Msaafu  aliyegombea urais kupitia Chadema na kuungwa mkono na mwamvuli wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, Edward Lowassa, amesema kuwa katika uchaguzzi mkuu ujao  atakwenda ikulu  bila ya kumwaga damu ya mtu yoyote kwa kuwa watanzania wanaimani naye.


Kauli hiyo aliitoa jana ilipowasili mkoani Iringa alipokwenda  kuzungumza na wafuasi wa chadema kwenye vikao vyao ndani vinavyoendelea nchi nzima juu ya kampeni ya kupinga uvunjwaji wa demokrasia nchini (UKUTA )


Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alisema kuwa licha ya kwamba uchaguzi ulikwisha  kupita lakini anaamni na watanzania wanaamini alishinda kwa kura nyingi lakini aliamua kukaa kimya  maana kila jambo linalotendeka mungu ana makusudi nalo


 “vijana wengi hawakuridhika na vijana walinifuata na kuniambia twende tukadai haki yetu lakin wataqnzania ndio walke wale tumeoleana sasa kuna haja gani mimi kwenda ikulu na damu za watanzania mikononi sikutaka hilo lakini napenda kuwaambia 2020 tunakwenda ikulu kwa kuwa sababu ya kwenda ikulu tunayo


Sababu moja wapo ya sisi kwenda ikulu ziko nyingi moja maeneo makubwa ya majiji wameshikilia wao na ndio maana anawataka madiwani wote walioko katika maeneo hayo  wafanye kazi kwa bidii ili wasiwaangushe watanzania waliowaamini na kuwapa dhamana ya kuwaongoza


Chama cha mapinduzi kimejeruhiwa ndio maana wanahangaia kuzuiya kila nifanyacho wananizuiya  mimi nilianza kufanya ziara zangu za kuwambia watanzania asante lakini ccm na serekali yake wameamua kunizuiya kila niendeko ili niseme  tu asante lakini nikenda huku polisi nikenda kule polisi  lakini natamani nimfikie kila mmoja hata yule ambaye hakunipigia kura lakini aliniwazia mema nataka nimfikie  nimwambie asante lakini wananizuiya sasa na nyie nawatuma kawambieni lowasa anasema asante sana .


Lowasa alisema kuwa sasa kazi iliyobaki ndani ya chama hicho ili kuweza kushika dola ni mkuhimu kupenda kushirikiana kwa kila jambo wafanyalo ili kuweza kujenga nguvu moja ya kulelekea ikulu kwa kuwa ninjiani nyeupe na tayari mtimishi wa mungu Nabii Tibi Joshua alishamwambia kuwa serekali ijayo ni serekali ya chadema hivyo hata yeyew anaamini kuwa itakuwa hivyo



 Hashim Juma Issa kutoka Baraza la Wazee Taifa  alisema kuwa jambo wanalofanya la kupinga uvunjwaji wa demokrasia nchini hawabahatishi na wala hawatishi  watu bali watatekeleza dhamira yao kwa kuwa wanataka haki itendeke ndani ya nchi bila ya kuvunja katiba ya nchi .


Alisema kuwa Amani na utulivu wa watanzania iko mikononi mwa watanzania wenye na wala haiko mikononi mwa chama chochote hivyo ni vyema vyama vya siasa vikaheshimu maamuzi ya watanzani na kuwapa uhuru wa demokraisa bila ya kuwatisha na kuvunja katiba ya nchi .


“Siku hiyo ikifika  ya sepetember 1 niwaombeni wote   fanyeni maandamano yenu kwa Amani na utulivu bila ya kufanya vurugu yoyote wala kugusa gari ya mtu wala kikombe cha mtu  kwa kuwa chadema ni watu wa Amani na sasa  huu ni mtihani wetu wa kwanza tuwaonyesha watanzania sisi sio watu wa vurugu bali tunataka haki etendeke bila ya kupendelea upande wowote ”






















0 maoni:

Chapisha Maoni