Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akikagua Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu wakati wa ziara yake hiyo ya kikazi hivi karibuni Agosti 2016.
DSC_6021
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akipata maelezo kwa msimamizi wa Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu. 
DSC_6025
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akiwaonyesha namna wanavyokiuka taratibu za ndani ya Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu
DSC_6028 DSC_6040
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akihoji namna ya mpangilio wa Maabara unavyokosewa na wasimamizi wa Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu
DSC_6047
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akielekeza namna ya Maabara inavyotakiwa iwe
DSC_6072
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla (kulia) akitoa maagizo kwa Viongozi wa Serikali na watendaji wa Hospitali hiyo kuhakikisha wanafanyia marekebisho mapungufu yote yaliyobainika ndani ya miezi mitatu yawe yamepatiwa ufumbuzi.
DSC_6106 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla akiagana na viongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Kishapu

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi  Kigwangalla amezitaka Maabara Nchini kuhakikisha zinafuata misingi na kanuni sahihi katika kuzingatia ubora  na ufanyaji.
Akiwa katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Shinyanga, Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla aliweza kukagua Maabara ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu  ambapo alibaini mambo mbalimbali yakifanywa bila kuzingatia taratibu sahihi za Mabara huku akiagiza Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wanarekebisha mapungufu hayo katika Maabara hiyo.
Miongoni mwa mambo ambayo alikuta katika Maabara hiyo ni pamoja na kutokuwa na taratibu za kiutendaji hasa kwa wafanyakazi wenyewe wa Maabara ambao walishindwa kuzingatia vigezo na msharti ambayo taratibu za Maabara zinahitaji.
Picha na Andrew Charle