Jumatatu, 29 Agosti 2016

MAHAKAMA YAMTANGAZA JOSEPH RYATA KUWA DIWANI HALALI KATA YA KWAKILOSA MANISPAA YA IRINGA

Postedy by Esta Malibiche on August 29.2016
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Iringa imemtangaza Joseph Ryata (Chadema)kuwa mshindi halali wa kiti cha udiwani wa  kata ya Kwakilosa katika Halmashuari ya Manispaa ya Iringa baada ya kutupa hoja zilizofikishwa mahakamani hapo kupinga ushindi huo.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Makazi Mfawishi wa mahakama hiyo David Ngunyale alisema upande wa mlalamikaji umesindwa kutoa ushahidi unaotosha kuishawishi mahakama  kutengua matokeo hayo ya uchaguzi wa 2015 kama ulivyodai.

Hakumu Ngunyale alisema  baada ya kupitia pande zote za mashidi tisa walioletwa na upande wa mlalamikaji na mashihidi saba waliofikishwa mahakamani hapo na upande wa mlalamikiwa , mahakama imeona hakuna ushahidi uliotosha kuishawishi  mahakama hiyo ili kuweza kutengua matokea yauchaguzi huo.

“Baada yakupitia hoja zote mahakama imeona  mlalamikaji hakuweza kuleta ushahidi unaotosha kuishawishi mahakama itenguematokea hiya,hivyo mahakamainamtangaza Joseph Ryata kuwa mshindi halali wa kiti hico cha udiwani”alisema Ngunyale.

Akizungumza mara baada ya hukumu hiyo wakili aliyekuwa akimwakilishi mlalamikia Alfred Mwakingwe alisema atakwenda kukutana na mawakili wenzake pamoja na mteja wake ili wajadili na kuona hatua za kuchukua.

Naye wakili wa upande wa utetezi Baranabas Nyalusi alisema mahakama imemtendea haki mteja wake na kushauri  wanasiasa kuwa na utaratibu wa kukubari matokea pindi wanapotangwa kuwa wameshindwa uchaguzi na kujipanga kwauchaguzimwingine.

Hamid Mbata ambaye alishindw akatika kesi hiyo alisema anasubiri apate hukumu iliyotolewa mahakamani hapo kwa maandishi na baada ya kuipitiana kuitafakari ataamua cha kufanya.

Naye Ryata ambaye pia ni Naibu Meya wa Halmashauriya Manispaa ya Iringa aliishukuru mahakama kwa kutenda haki na kuahidi kufanya kazi zaidi ya ilivyokuwa mwanzo kwa kuwa alipoteza muda  mwingi mahakamani alikokuwa anakwedna kusikiliza kesi.

MWISHO

0 maoni:

Chapisha Maoni