Jumatatu, 22 Agosti 2016

KATIBU TAWALA WA WILAYA YA IRINGA JOSEPH CHITINKA AMEWASIHI VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO ILI KUJIINGIZIA KIPATO

Postedy by Esta Malibiche on August 22.2016 in News with No Comment
Katibu tawala wa Halmashauri ya Iringa Joeph Chitinka akizungumza na vijana [hawapo pichani\katika semina ya mafunzo kuhusu ujasiliamali kwa vijana qwaliohitimu chuo,wasio na ajira na wajasiliamali iliyofanyika katika ukumbi wa siasa ni kilimo mjini Iringa

Na Esta Malibiche
Iringa
KATIBU tawala wa Wilaya ya Iringa Joseph chitinka amewasihi Vijana kuchangamkia fursa zilizopo kwa kujiajili wenyewe  ili waweze kuondokana na dhana ya kuisubiri serikali iwaajiri
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akifungua semina ya mafunzo ya ujasiliamali kutoka shirika la Right way for development [Riwade]ambalo linafanya kazi ya kuwasaidia vijana wasio na ajira kufanya kilimo,ufugaji,uvuvi kuwa ni moja ya ajira.Mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani hapa na kuhudhuriwa navijana kutoka wilaya Kilolo,Mufindi,Iringa vijijini,Manispaa ya Iringa na Halmashauri ya mji wa Mafinga.
Mafunzo hayo yaliwahusisha vijana  ambao bado hawajapata ajira bado baada ya kuhitimu vyuo mbalimbali,wakulima na wafugaji na wajasiliamali.
Chitinka alisema kuwa serikali pekee haiwezi kutoa ajira kwa vijana wote wanaohitimu vyuo nchini,bali  vijana wanatakiwa kujiajili wenyewe kwa   kuchangamkia fursa zilizopo hasa katika kilimo ili waweze kujikwamua kimaishana kujipatia maendeleo.Pia alisema  ili mjasiliamali aweze kupiga hatua anatakiwa ajitambue  mwenyewe pamoja na kutambua mazingira yanayomzunguka.
‘’’’’ Mkoa wa Iringa una utajili wa ardhi yenye rutuba ,endapo vijana watachana na tabia ya kukaa vijiweni asubuhi na kucheza michezo isiyo na manufaa kwao  na kuamua kufanya kazi kwa bidii katika kilimo wataweza kujikomboa na wimbi la umasikini ‘’’’alisema Chitinka
Tunapata matumaini makubwa na Serikali iliyopo madarakani kutokana na kuhimiza kila mmoja wetu afanye kazi kwa juhudi.Tuwekeze kwenye vitu vya msingi ambavyo vinaweza kutuletea maendeleo endapotukipata mikopo kutoka Riwade.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Riwade Ayubu Masau akiendesha semina kwa vijana wahitimu vuyuo vikuu wasio na ajira alisema kuwa  vijana waliowengi wamejitengenezea dhana ya kuwa mara wamalizapo vyuo wanasubiri serikali iwaajiri na si kujiari.
Ile dhana ya kuajiliwa inatakiwa iondolewe miongoni mwa vijana na hatimae waweze kujiajili kwa kutumia fulsa zilizopo na zinazotolewa na serikali pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali’’’’’
Alisema  tatizo kubwa la ajira kwa vijana linatokana na Elimu tunayoipata,hivyo kwa kupitia shirika la Riwade vijana wanatakiwa kusimama kwa kujiajili bila kusubiri kuajiliwa na serikali pekee
Masau alisema kupitia sekta ya kilimo,uvuvi na ufugaji inaweza kupunguza  changamoto kubwa ya ajira kwa vijana nchini endapo vijana watajitambua na kukaa pamoja kwa kupanga mikakati yao mara  wamalizapo vyuo.
‘’’’’’Lengo la Riwade ni kuwasaidia vijana wasio na ajira waweze kufanya kilimo,ufugaji,uvuvi wa kisasa ulioendelevu na mazingira kuwa ni ajira tosha inayoweza kumkomboa kijana.Pia inawahusisha wakulima katika ngazi zote ili kuweza kushirikiana katika kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya kilimo,uvuvi, ufugaji na  mazingira kwa ujumla.
Alisema kuwa dira ya Riwade ni kuziboresha huduma za jamii ambazo zinapelekea ukuaji wa hali ya kiaisha kwa wananchi.Pia inatengeneza na kutoa fursa kwa watanzania wote ili waweze kupata Elimu ya ujasiliamali na namna ya kutengeneza mitaji ya ukuaji endelevu wa kijamii na kiuchumi.
Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo,Josiah Kifunge ni muhitimu wa chuo kikuu Iringa [Tumaini] toka mwaka 2012 hadi sasa hajapata ajira serikalini na, ameamua kujishugulisha na ujasiliamali katika kilimo, alilishukuru shirika la Riwade na kusema kuwa mafunzo waliyoyapata watayatendea kazi ipasavyo.
‘’’’’Mimi binafsi baada ya kuhitimu chuo nilikuwa na wazo la kuajiliwa lakini nimeakaa zaidi ya miaka mine sijapata ajira,nimeamua kujiajiri kwa kujikita katika kilimo.Zaidi nalima mazao ya mbogamboga  na nimeweza kupiga hatua ‘’’’
 Nimefundisha semina nyingi na nimehudhuria semina nyingi za ujasiliamali,hii ya leo imeweza kugusa mahitaji ya vijana wahitimu wasio na ajira na kuwawezesha kujiajiri pasipo kusubiria kuajiliwa.Riwade wamejibu changamoto za vijana waliowengi wasio na kipato.
Kifunge aliongeza kuwa  semina nyingi za ujasiliamali  wakufunzi huwa wanatoa mafunzo na kuwaacha washiriki wake njia panda bila ya kuwapa mwongozo na namna ya kujikwamua,lakini semina iliyotolewa na Riwade imeweza kuwaunganisha kwa pamoja.








Mkurugenzi wa shirika la RIWADE  Eng.Ayubu Masau akitoa semina elekezi kwa vijana [hawapo pichanai]kuhusu kujialiri 








 Semina ikiendelea huku washiriki wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizoendeshwa na mkurugenzi wa RIWADE,Eng.Ayubu Massau



Mkurugenzi wa RIWADE Eng.Ayubu karikati mwenye shati la kitenge akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa semina kutoka Manispaa ya Iringa
Mkurugenzi wa RIWADE Eng.Ayubu karikati mwenye shati la kitenge akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa semina kutoka wilaya ya kilolo
Mkurugenzi wa RIWADE Eng.Ayubu karikati mwenye shati la kitenge akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa semina kutoka Wilaya ya Mufindi
Mkurugenzi wa RIWADE Eng.Ayubu karikati mwenye shati la kitenge akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa semina kutoka Halmashauri ya Mji wa Mafinga
 Mkurugenzi wa RIWADE Eng.Ayubu karikati mwenye shati la kitenge akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa semina kutoka Halmashauri Iringa jimbo la Isimani

Mratibu wa RIWADE  Mkoa wa Iringa Vumilia,akiwa na mshiriki wa semina Josiah Kifunge, muhitimu katika chuo kikuu Iringa[Tumaini]ambae ni mjasiliamali wa kilimo cha mbogamboga.
Baadhi ya washiriki kutoka kila wilaya zilizopo mkoani Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa RIWADE  Tanzania Eng.Ayubu Masau 
Picha zote na Esta Malibiche[KALI YA HABARI BLOG]



















0 maoni:

Chapisha Maoni