Jumapili, 28 Agosti 2016

MBUNGE WA VITI MAALUM CHADEMA RISALA KABONGO AONGOZA HARAMBEE KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENABOISHU ARUMERU MKOANI ARUSHA

Postedy by Esta Malibiche on August 28.2016 in News with No Comment
Mbunge Risala akivishwa kitenge na walimu mara baada ya kuwasili katika viwanja vya shule ya sekondari Enaboishu iliypo Arumeru Arusha



Vikundi mbalimbali vya sanaa vikiendelea kutumbuiza











Mbunge wa viti maalum chadema Risala Kabongo amekusanya kiasi cha Mill.18.2 katika harambee ya  yakuchangia  maendeleo katika ya  Shule ya sekondari Enaboishu  Arumeru iliyoko mkoani Arusha tarehe 27.8.2016.
Harambee hiyo iliambatana na sherehe ya kuadhimisha miaka 50 ya shule hiyo toka kuanzishwa kwake,pamoja na mahafari ya 48 ya kidato cha nne.
Mbunge Kabongo na familia yake walichangia kiasi cha Tsh.5 mill.na alifanikiwa kukusanya kiasi cha Tsh.13.2,hivyo kufikia jumla ya kiasi cha Ts.18.2 mill.
Aliwashukuru wananchi na wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo kwa kumuunga mkono katika harambee hiyo aliyoiongoza akiwa mgeni rasm.
Alisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya bweni la wasichana,vyoo vya kisasa,bwalo la chakula na maktaba ya kisasa,ambapo kiasi hicho cha fedha kilichopatikana kitasaidia kutekeleza mahitaji hayo.
Pia aliwasihi wanafunzi kuzingatia masomo,kusoma kwa bidii ili waweze kukamilisha ndoto,na kuwataka  kujiepusha na viashiria vinavyoweza kukatisha masomo yao na kuharibu ndoto zao za baadae.


















0 maoni:

Chapisha Maoni