Jumatano, 17 Agosti 2016

Mabalozi waendelea kutoa salamu za pole msiba wa Marehemu Mzee Aboud Jumbe

omb1
Balozi wa Uganda nchini Tanzania Bi. Dorothy Samali Hyuha akisaini kitabu cha maombolezo na kutoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekua Rais wa Pili wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
omb2
Mwakilishi wa Ubalozi wa Nigeria nchini Bi. Abiola Sherif Deluya akitoa salamu za pole katika kitabu maalumu kilichopo katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa Luthuli, Jijini Dar es Salaam leo.
omb3
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Bw.  Jassem Al Najem ni miongoni mwa mabalozi waliotembelea Ofisi ya Makamu wa Rais leo na kutoa salamu za pole kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar.
omb4
Balozi wa Palestina nchini Tanzania Bw. Hafen Shabit akisoma dua mara baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo kilichopo katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa Luthuli, jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais

0 maoni:

Chapisha Maoni