Ijumaa, 19 Agosti 2016

DKT.KIGWANGWALLA AWAPA MIEZI SITA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUWA NA THEATRE ZENYE KUFANYA KAZI

Postedy by Esta Malibiche on August 2016

indexMeatu,Simiyu
Waganga wakuu wa mikoa na wilaya wote nchini wametakiwa  kuwa na vyumba vya upasuaji ‘theate’ zenye kufanya kazi ipasavyo kwenye vituo vyote vya afya kwenye maeneo yao ndani ya miezi 6.
Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri wa Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Hamis Kigwangwalla mara baada ya kutembelea kituo cha afya cha Mwandoya kilichopo Meatu mkoani Simiyu kilichopo umbali wa kilometa 60 kutoka hospitali ya wilaya ya meatu
“Hawa wa Meatu wenyewe wana kituo cha Afya Mwandoya wamekipa uwezo wa kufanya upasuaji kituo hiki,Wamenunua vifaa, wameajiri hadi Daktari (MD) kwa ajira ya muda kwa ajili ya kufanya kazi pale”.
Aidha, alisema  Kituo hicho kimefanya takriban operation 40, zote salama Kwa asilimia 100. Wamepunguza msongamano Mwanhuzi na wamepeleka huduma nyeti na za kuokoa maisha Karibu zaidi na wananchi, ukizingatia huku hakuna barabara za lami na hakuna gari la kubebea wagonjwa (ambulances).
“Leo nimeamua kuchukua uamuzi wa kutoa agizo kali kabisa toka nimeteuliwa. Najua litazua maswali, lakini litaokoa maisha ya wanawake wajawazito wa nchi yetu (CEmOC) na wananchi wengine, Nitalitetea. Nitalisimamia”alisisitiza dkt.Kigwangwalla.
“Wiki iliyopita nilitembelea Manispaa ya Ilala, kwenye vituo vya afya vitatu nilivyotembelea hakukuwa na theatre yenye kufanya kazi. Kwa mujibu wa sera ya afya ya Tanzania, ‘kituo cha afya’ kitakuwa na hadhi hiyo kama kina uwezo wa kufanya upasuaji. Vinginevyo hiyo ni zahanati. Mara nyingi watendaji hawa wamekuwa wakijificha kwenye kichaka cha ‘hatuna fedha’, wengine wakiomba fedha kutoka serikali kuu”.
Hata hivyo alimuuliza Mkurugenzi wa Ilala, anakusanya shilingi ngapi Kwa mwezi, akasema bilioni 6. Nikamuuliza unadhani ni shilingi ngapi kuwa na theatre yenye kufanya kazi? Akakosa jibu. Nikampa miezi 6 awe na theatre zenye kufanya upasuaji.
Naibu waziri huyo anasema jana ametembeleaMkoa wa Shinyanga na Simiyu na kukutana na tatizo hilo hilo alipokuwa Kishapu, Shinyanga na Mwanhuzi, Simiyu.
“Nimesema sababu za kuwa Halmashauri hazina pesa huku zinakusanya mamilioni ambayo wanayatumia bila kuainisha matatizo ya msingi ya wananchi hazikubaliki, Leo iwe mwisho”. Nawaagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini washirikiane na Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya wajue watakavyofanya wahakikishe wanafungua huduma za upasuaji kwenye vituo vyote vya afya nchini ndani ya miezi sita (6).
“Baada ya miezi hiyo sita mimi mwenyewe na timu yangu ya kurugenzi ya ukaguzi na uhakiki ubora wa huduma za afya (inspectorate and quality assurance) tutasambaa nchi nzima kukagua huduma hizi na pale ambapo hatutozikuta tutakishusha hadhi kituo hicho kutoka ngazi ya ‘kituo cha afya’ na kuwa ngazi ya ‘zahanati’ sambamba na kuwashauri wenzetu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwa wakuu hao wa idara wameshindwa kutekeleza majukumu yao na hivyo wawashushe vyeo”. “Nitasimamia uamuzi huu Kwa nguvu zangu zote. Sababu ni kwamba ninajua faida yake. Ninajua Mungu atafurahi, atanibariki”.
Wakati wa Bunge la bajeti wanaharakati wa haki za wanawake na Watoto waliwahamasisha Wabunge wawashughulikie Kwa ajili ya suala hili. Wakawa washawishi wabunge  kuwa kwa siku takwimu za  vifo vinavyotokana na sababu za uzazi ni sawa na ‘coaster’ moja ipate ajali na iue watu wote! Wabunge waligeuka mbogo. Japokuwa namba hizi zilikuwa zilizidishwa, walifikisha ujumbe kwetu mawaziri. Kwamba lazima tufanye kitu tofauti kwenye eneo hili. Mimi naanza kuchukua hatua. Vifo vitokanavyo na uzazi havikubaliki! Alisema Naibu waziri wa afya.

0 maoni:

Chapisha Maoni