Jumatano, 17 Agosti 2016

MKUU WA MKOA WA IRINGA AMINA MASENZA AWAAGIZA VIONGOZI WA DINI KUHAMASISHA WAUMINI WAO KULIPA KODI



 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwa katika kikao maalum
 Meneja wa TRA mkoa wa Iringa Joseph Kalinga akizungumza na viongozi wa dini katika kikao maalum





Viongozi wa dini waliohudhuria kikao wakisikiliza kwa makini





Na Esta Malibiche
Iringa
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka viongozi wa dini mkoani hapa kuwahubiria waumini wao kuhusu wa kulipa kodi kwa kila mfanyabiashara,na umuhimuwa kudai risiti  kwa kila mnunuzi .
Akizungumza jana katika kikao maalum cha viongozi wa dini mbalimbali mkoani Iringa , Mkuu wa mkoa alisema kuwa nchi nyingi  zilizoendelea duniani,wafanyabiashara wake  hawakwepi kulipa kodi,na wanalipa kwa wakati.
‘’’’Ninawaomba viongozi wa dini mkoani hapa kwa pamoja tushirikiane ili kuwaelimisha wananchi katika vyumba vya ibada na vikao vyetu tunavyofanya huko,marawanapouza watoe risiti pamoja na wanaponunua wadai risiti ili kuzuwia ukwepaji wa kulipa kodi’’’
‘’Kama kweli Watanzania tunataka kuyaona mabadiliko anayofanya mh.Rais kila mfanyabiashara anatakiwa kulipa kodi pasipo kukwepa.Na mtu yeyote anaekwepa kulipa kodi maana yake huyo mtu ni mwizi.Iko haja ya kuopambana na wakwepa kodi ili mkoa wetu na Taifa kwa ujumla liweze kusonga mbele……alisema Masenza
Masenza aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa serikali kutoa taarifa juu ya wafanyabiashara wasitoa risti baada ya kununua bidhaa.
Aidha mkuu huyo wa mkoa aliitaka TRA   kuhajkikisha wanayafikia makundi mbalimbali wakiwemo waendesha pikipiki [bodaboda] na  kutoa Elimu ya kulipa kodi, ili kila mwananchi aone umuhimu wa kulipa kodi
‘’Mh .Rais katoa maagizo kutowabughudhi wafanyabiashara wadogowadogo kama akina mama wanaouza mbogamboga wasilipishwe kodi.Ila wale wanaosambaza chakula mashuleni ni lazima walipe kodi.Kiongozi yeyote wa dini asiruhusu mfanyabiashara kusambaza chakula shuleni kwake bila kutoa risiti.’’’
Awali viongozi wa dini walihoji kuhusu TRA walivyojipanga Elimu kwa mlipa kodi,ambapo Mchungaji  Kanani Baraka za bwana Eliya wa kanisa la Soloam ministry Internation ambae ni mkuu wa kanisa hilo kanda ya kusini alisema kuwa Elimu ni muhimu sana kutolewa kwa kina kwa wafanyabiashara ili kila mfanyabiashara anapotoka nyumbani atambue faida inayotokana na matumizi ya mashine ya kutolea risiti.
Endapo Elimu yenye ufahamu ya kutosha haitatolewa kwa jamii matokeo yake hakutakuwa na mwamko mkubwa wa wafanyabiashara kuhamasika kununua mashine hizo na kuzitumia.Pia naomba kuhoji mikakati iliyowekwa na TRA  kuhakikisha mashine za EFD zinakuwa na ulinzi qwa kutosha kutokana na sheria iliyopo kuhusu  usalama wa mtumiaji wa mashine hizo pamoja na uangalizi utakaosababisha  zisichezewe na matapeli’’’.’’’’’alisema
Sheikh  kaimu chalamila na Abdusalaam Ahamed Ayoub kutoka dhinurey Islam foundation walihoji na kunae kusema kuwa  TRA inatakiwa kuwa na mpango mahususi  kuhakikisha kila mwananchi wa Iringa atambue kwamba asipopokea risiti ni hatua zipi za kinidhamu zinastahili achukuliwe,Pia anatakiwa atambue kuwa kutoa  risiti na kutopokea ni jambo la kisheria ambalo limepangwa na serikali na si vinginevyo
‘’’’Ni muhimu sana TRA watambue ni wanunuzi wangapi wanofahamyu kwambani lazima kudai risiti baada ya kunu nua.Na niwanunuzi wangapi wanaofahamu kwamba ukikataa kupokea risitri unaweza kuchukuliwa hatua gani.’’’’’alisema
Kawa upande wake Meneja wa TRA mkoa wa Iringa Joseph Kalinga akijibu maswali kutoka kwa viongozi wa dini alisema kuwa adhabu ya mwananchi atakaeshindwa kudai risiti mara anaponunua vifaa dukani ni Tsh.30,000 kwa mujibu wa sheria na mwaka 2016 inavyosema na kusisitiza hilo.
Kalinga alisema kwa upande wa Elimu kwa wafanyabiashara imetolewa vya kutosha kuanzia mjini hadi vijijini
‘’’Tumefanya semina na watu wanaouza vifaa vya ujenzi,wafanyabiashara wa maduka ya kawaida nay a jumla,kama jitihada hiozo zimegoma tuna mikakati madhubuti tuliyoipanga kupambana nao.Pia nawaomba viongozi wetu wa dini tusaidiane kutoa Elimu kwawauminikuhusu kudai risiti na kutoa risiti ili wafanyabiashara waweze kulipa kodi’’’alisema
Akifafanua kuhusu faida zinazotokana na kutumia mashine za EFD ,Meneja huyo alisema kuwa,mashine zina  uhakika wa usalama wa taarifa za biashara kutokana na kutunzwa katika kifaa maalum.Inaahirisha kufanya makadirio sahihi na haki.
Alisema kuwa mashine ni zaidi ya risiti, inaweza kutumika katika shughuli zingine kama kufanya mauzo na kutuma taarifa mbalimvali,na zinatoa risiti ambazo ni ngumu kuzigushi.
Aliongeza kuwa lengo la serikali kuwataka wafanyabiashara watumie mashine hizo  ni kuiwezesha serikali kupanga mipango ya kiuchumi kulingana na mapato ya ndani.Kuimarisha na kuboresha kumbukumbu za biashara na kutoa haki katika makadilio ya ulipaji kodi
‘’’’’’Kuna sheria mbalimbali za kodi ya ongezeko la thamani ya 1997,kama ilivyorejewa mwaka 2006.[kanuni za mwaka 2010].Sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004,kama ilivyorejewa mwaka 2006[kanuni za mwaka 2012]Pia kuna sheria ya usimamizi wa kodi ya mwaka 2015[kanuni za mwaka 2016]’’’’’’alisema
MWISHO







0 maoni:

Chapisha Maoni