Ijumaa, 4 Novemba 2016

UONGOZI WA MANISPA YA DODOMA WATAKIWA KUKAMILISHA UJENZI WA MADARASA SHULE YA MSINGI CHANG’OMBE.

Posted by Esta Malibiche on Nov 4,2016 in NEWS

4

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI)  Mhe. Selemani Jafo akimpa maelekezo  Afisa Mipango Miji  wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma  Bw Clemence Mkusa  juu ya ujenzi wa zahanati ya kata ya Chang’ombe wakati alipotembelea eneo ambalo  zahanati itajengwa wakati wa ziara yake aliyoifanya katika kata ya Chang’ombe iliyofanyika terehe 03 Novemba, 2016.
1
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akimpa maelekezo Diwani wa kata ya Chang’ombe Bw. Bakari Fundikira juu ya ujenzi wa soko jipya la Chang;ombe wakati alipofanya ziara ya kukagua shughuli mbalimbali zinazotekelezwa katika kata hiyo iliyofanyika tarehe 03 Novemba, 2016.
2
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Seleman Jafo akipokea taarifa za maendeleo ya ujenzi wa soko la Chang’ombe B kutoka kwa Mtendaji wa kata ya Chang’ombe Bi. Asha Juma wakati alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa soko jipya la Chang’ombe B  unaofanywa katika kata ya Chang’ombe mjini Dodoma aliyoifanya leo tarehe 03 Novemba, 2016.
3
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Seleman Jafo akiwapa mikono wanafunzi wa shule ya msingi Chang’ombe baada ya kuwapa taarifa juu ya ujenzi wa madarasa na ukarabati wa majengo ya shule yao wakati wa ziara aliyoifanya katika shule hiyo leo tarehe 03 Novemba, 2016.


5
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akikagua  jengo la ofisi ya Mtendaji wa kata ya Chang’ombe linaloendelea kujengwa wakati wa ziara aliyoifanya katika kata ya Chang’ombe  kukagua shughuli mbalimbali za kimaendeleo zinazofanywa katika kata hiyo.
6
Naibu Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akiwasalimu wanafunzi wa shule ya msingi Chang’ombe B iliyopo mjini Dodoma  wakati alipofanya  ziara ya kukagua shughuli mbalimbali za kimaendeleo zinazofanywa katika ziara hiyo.
7
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR-TAMISEMI) Mhe. Seleman Jafo akipokea taarifa za maendeleo ya ujenzi wa shule ya Msingi Chang’ombe B, iliyopo katika halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Shule  hiyo Bi.Nelly Kinyaga alipotembelea shuleni hapo wakati alipofanya  ziara ya kukagua shughuli mbalimbali za kimaendeleo zinazofanywa katika kata hiyo.
Na. Nasra Mwangamilo, Silvia Hyela
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameuagiza Uongozi wa Halmashauri ya  Manispaa ya Dodoma kuhakikisha inakamilisha ujenzi na ukarabati wa  vyumba vya madarasa ya shule ya msingi Chang’ombe, ifikapo tarehe 10 Januari, 2017 kabla ya msimu wa masomo kuanza.
Mhe. Jafo alisema serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) imetoa jumla ya shilingi Milioni 192 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa na ukarabati wa majengo machakavu katika shule ya msingi Chang’ombe na kuwataka watendaji hao kutumia vizuri fedha hizo zilizotolewa na serikali.
Mhe. Jafo alitoa agizo hilo leo tarehe 03 Novemba, 2016 wakati alipofanya ziara ndogo ya kutembelea Kata ya Chang’ombe ambapo katika ziara hiyo alibaini  changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo zikiwemo upungufu wa madarasa na matundu ya vyoo.
“Natoa agizo kwa Afisa Mipango na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa, ifikapo tarehe 10 Januari, 2017, ujenzi wa majengo haya uwe umeshakamilika na muhakikishe shule yote inakuwa mpya. ”  Alisisitiza Mhe. Jafo.na kuongeza kuwa angependa kazi hiyo ifanyike ndani ya muda na kutojengwa chini ya kiwango cha ubora.
Aidha,  Naibu Waziri  Jafo alionyesha kutoridhishwa na taarifa za ujenzi wa zahanati ya kata ya Chang’ombe ambayo taarifa zilizotolewa zilionyesha kuwa hazikuwa sahihi ukilinganisha na idadi ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo.
“Sijaridhishwa kabisa na ujenzi unaoendelea katika zahanati hii na siamini kama kulikua na usimamizi mzuri, nataka niletewe taarifa inayoambatana na taarifa ya mkandarasi aliyehusika na ujenzi pamoja na mchakato wa manunuzi ya vifaa na maendeleo ya ujenzi ili nijiridhishe na suala hili ”aliagiza Naibu Waziri  Jafo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Jafo alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa Manispaa ya Dodoma na kuwataka  kufanya kazi kwa kuzingatia umuhimu wa mahitaji ya wananchi na kuyawekea kipaumbele mambo ya msingi ikiwamo huduma za afya na elimu lengo likiwa ni kuhakikisha watumishi wa Serikali za Mitaa wanakua watumishi wa mfano kwa utendaji mzuri.

0 maoni:

Chapisha Maoni