Jumanne, 15 Novemba 2016

NAIBU WAZIRI WA HABARI AITAKA KAMATI YA URASIMISHAJI KUHUSU SEKTA YA UBUNIFU KUWEKA MFUMO RASMI WA KUWATAMBUA WADAU WAKE

Posted by Esta Malibiche on Nov 15,2016 in NEWS

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura(kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara  hiyo Bibi.Nuru Millao(katikati) alipowasilia katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo Jijini Dar es Salaam tayari kwa kufungua Warsha ya Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya Ubunifu iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania,kushoto ni Katibu Mtendaji wa Bodi hiyo.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura(kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya hiyo Bibi.Nuru Millao(kushoto) alipowasilia katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo tayari kwa kufungua Warsha ya Kamati ya Urasimishaji wa sekta ya Ubunifu iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michszo  Bibi.Nuru Millao(kushoto) akiongea kabla ya kumaribisha Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe.Anastazia Wambura (katikati) wakati wa ufunguzi wa warsha ya Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya Ubunifu iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi.Joyce Fissoo.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura(katikati) akiongea na wajumbe wa Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya ubunifu wakati wa ufunguzi wa warsha ya wajumbe hao leo Jijini Dar es Salaam,kulia kwake ni   Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya hiyo Bibi.Nuru Millao na kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi.Joyce Fissoo.

. Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma ya Ufundi kutoka Bodi ya Filamu Tanzania Bw.Romanus Tairo akiwasilisha mada kuhusu  sekta ya ubunifu wakati wa warsha ya kamati ya urasimishaji ya sekta hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt.Mona Mwakalinga(kushoto) akifafanua jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu  uwezo wa sekta ya filamu katika kuchangia uchumi katika warsha ya kamati ya urasimishaji wa sekta ya ubunifu leo Jijini Dar es Salaam,kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Hakimiliki na Shiriki Tanzania (COSOTA).

Mkurugenzi Msaidizi Tathmini na Ufuatiliaji Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo  Bw.Bernard Lubobo akiuliza swali katika warsha  ya kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya Ubunifu iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Sanaa kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi.Leah Kihimbi akichangia hoja katika warsha ya Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya ubunifu leo Jijini Dar es Salaam iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania ambapo mada mbalimbali ziliwasilishwa.

Wajumbe wa Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya Ubunifu wakifuatilia  kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji leo Jijini Dar es Salaam.

Wajumbe wa Kamati ya Urasimishaji kuhusu sekta ya Ubunifu wakiimba wimbo wa kuhamasisha ushirikiano katika warsha iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania ambapo mada mbalimbali ziliwasilishwa na wawezeshaji leo Jijini Dar es Salaam.

Picha/Habari Na Lorietha Laurence
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura ameitaka kamati ya urasimishaji sekta za ubunifu kuweka mfumo rasmi wa kuwatambua wadau wa sekta hizo ili waweze kuwasimamia.

Mhe. Anastazia ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua warsha iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu Tanzania ambapo alieleza kuwa kwa kuwepo kwa mfumo rasmi wa kutambaua  sekta hizo kutarahisisha kuwatambua wasanii katika makundi mbalimbali.

“Sekta ya ubunifu ni pana na muhimu katika kukuza pato la mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla hivyo ni muhimu kurasimisha kwa kuwepo mfumo rasmi wa kuitambua” amesema Mhe. Anastazia.

Anaongeza kuwa kwa kutambua umuhimu wa sekta ya ubunifu Rais wa awamu ya tano Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliamua kufuata ilani ya chama cha Mapinduzi katika kuunda Wizara ambayo inajihusisha na mambo ya sanaa.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao amesema kufuatia warsha hiyo anaamini itasaidia kamati ya urasimishaji kujipanga katika kusimamia kazi za filamu na muziki ili kuwa ajira rasmi yenye kuingizia watu kipato.

“Mbali  ya sekta hii ya ubunifu kuwa rasmi pia itasaidia katika kusambaza elimu kwa umma kuhusu mchango unaofanywa na sekta hiyo katika kukuza uchumi na kuongeza ajira nchini” alisema Bibi. Nuru.

Aidha Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo ameeleza kuwa warsha hiyo ipo katika kuwajengea uwezo wanakamati katika kuimarisha uelewa na kuifanya sekta ya ubunifu kuwa rasmi.

Kwa upande wake Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Mona Mwakalinga amefurahishwa kuona Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inathamini mchango wa kazi zote za ubunifu kwa kutaka kuzirasimisha kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuinua kazi za ubunifu na kuzifanya kutumika zaidi nje ya nchi.

0 maoni:

Chapisha Maoni