Jumamosi, 26 Novemba 2016

JAFO AWATAKA MAAFISA ELIMU KUPANGA MUDA WA KUSIKILIZA KERO ZA WALIMU NA KUZITATUA.


Posted by Esta Malibiche on Nov 26,2016 in NEWS
gon1
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI  Selemani Jafo akisaini kitabu cha wageni shule ya sekondari Segera, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. Wiliam Makufwe na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe.
gon2
Picha ya pamoja ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi  Selemani Jafo na walimu wa shule ya sekondari ya Segera.
gon3
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni William Makufwe akitoa utambulisho mfupi kwenye ukumbi wa Halmashauri.
gon4
Baadhi ya watumishi wa halmashauri ya Handeni
gon5
Viongozi wakisikiliza kwa makini maagizo ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Selemani Jafo.
………………………………………………………………………….
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),SelemanI Jafo amewataka maafisa elimu kupanga muda wa kusikiliza kero za walimu na kuzitafutia ufumbuzi ili kuongeza morali ya walimu kufundisha.
Jafo ametoa agizo hilo alipokuwa akiongea na walimu wa shule ya sekondari Segera iliyopo wilayani Handeni, katika ziara yake aliyoifanya Wilayani Handeni na Mkoa wa Tanga. Amesema wapo baadhi ya Maafisa elimu ambao wanajifanya kuwa ni Miungu watu linapokuja suala la kusikiliza na kutatua kero za walimu.
“Najua wapo wapo walimu wanaotembea umbali mrefu kufuata huduma makao makuu ya Halmashauri kwa wakubwa wao mara nyingi wameshindwa kutatuliwa kero zao hali inayopelekea usumbufu, Kuanzia leo napiga marufuku tabia hiyo,”amesema Jafo.
Amesisitiza Maafisa elimu hao wapo kwa lengo la kuwasikiliza walimu na kuwasaidia kutatua kero zao ili waweze kujikita katika ufundishaji wa wanafunzi.
Kadhalika, amebainisha walimu ni watu muhimu sana nchini ila wamekuwa wakikatishwa tamaa na utendaji wa baadhi ya maafisa elimu.
Ameongeza kuwa kero kubwa ya walimu ni kutokupanda madaraja kwa wakati na kutopata stahiki zao ikiwa ni pamoja na posho za likizo,uhamisho na madai mengine.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Jafo ameagiza Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kukamilisha miradi yote ya SEDP-II ambayo haijakamilika kuhakikisha inakamilika kabla au ifikapo desemba 20, mwaka huu.
“Katika kusimamia miradi hiyo na miradi ya maendeleo kwa ujumla kila mtu lazima atimize wajibu wake na kuhakikisha fedha iliyotengwa na kutolewa inatumika vizuri na thamani fedha (value for money) inaonekana,”amesema Naibu Waziri Jafo.

0 maoni:

Chapisha Maoni