Jumatatu, 14 Novemba 2016

Qatar Airways yachangia madawati shule ya msingi Chanzige B, Kisarawe




Kampuni inayotoa huduma ya usafirishaji wa anga Qatar Airways nchini Tanzania imechangia madawati 100 katika shule ya msingi Chanzige B, iliyopo wilayani Kisarawe, mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya mradi wa kusaidia juhudi za serikali kupitia mpango wa kuondoa uhaba wa madawati nchini kwa shule za msingi pamoja na sekondari hii ni pamoja na sehemu ya kurudisha shukrani kwa jamii.
Mkabidhiano hayo yamefanyika katika viwanja vya shule hiyo leo Novemba, 14 katika viwanja vya shule hyo ambayo pia yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo mbunge wa Kisarawe na Naibu Waziri wa ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh.Seleman Jafo aliyekuwa mgeni rasmi pamoja, meneja wa Qatar airways Tanzania, Basek Haydar, wafanyakazi wa Qatar na wawakiishi kutoka ofisi ya Doha pamoja na Dk. Amon Mkoga ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Amon Mkoga Foundation, bodi ya wakurugenzi, walimu wa shule hiyo, wazazi na wanafunzi.
Akizungumza katika makabidhiano ya madawati hayo, Meneja wa Qatar Airways, Basek Haydar amemwakikishia naibu waziri Jafo kuwa wataendelea na mpango wa kusaidia jamii kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania kuinua na kuimalisha sekta ya elimu nchini.
Kwa upande wake naibu waziri Jafo ameipongeza Qatar Airways kwa msaada huo kwani umewezesha kupunguza kero kwa wanafunzi waliokuwa wakikaa chini, hata hivyo amewaomba uongozi wa shule hiyo kuangalia uwezekano wa kugawa madawati hayo shule jirani pale wanapoona panafaa kutokana na uhitaji uliopo.

0 maoni:

Chapisha Maoni