Jumatano, 30 Novemba 2016

KIWANGO CHA UFAULU MTIHANI WA DARASA LA SABA 2016 MKOA WA IRINGA CHAONGEZEKA NA KUFIKIA ASILIMIA 99.5

Posted by Esta Malibiche on Nov 30 ,2016 In NEWS
Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu akizungumza na wandishi wa Habari[Hawapo pichani]katika kikao cha kutangaza matokeo ya Mtihani wa darasa la saba mwaka 2016 kilichofanyika ukumbi wa Siasa ni Kilimo Halmashauri ya wilaya ya Iringa,Mkoani Iringa.


Na Esta Malibiche

Iringa

Kiwango cha ufaulu wa mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi 2016 Mkoani Iringa kimeongezeka kutoka wastani wa 82.8% mwaka 2015  hadi kufikia 99.5% mwaka 2016.

Akizungumza na wandishi wa Habari katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo uliiopo katika Halmashauri ya Wialaya ya Iringa,Katibu Tawala wa mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu alisema

Ayubu lisema ongezeko hilo ni mafanikio makubwa ambayo yameufanya mkoa kushika nafasi ya 3 kitaifa kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara.

‘’’’Ongezeko la ufaulu linaleta changamoto mpya ambayo kuwa na madarasa na madawati ya kutosha kwa idadi ya wanafunzi wote.’’’Alisema Ayubu

Akichanganua matokeo hayo alisema mwaka 2016 mkoa ulikuwa na watahiniwa 21,270 waliosajiliwa kufanya mtihani,  ambapo waliofanya mtihani walikuwa watahiniwa 21,177 ikiwa ni sawa na 99.5% namwa 2015 waliofaulu mtihani ni watahiniwa 17,587  sawa na 82.8%.

‘’’’Halmashauri ya mji wa Mafinga imeweza  kuongeza kiwango cha ufaulu ambapo Mafinga imeweza kushika nafasi ya nne kitaifa wakati Kilolo imeongeza ufaulu kutoka kwa 13%, Wilaya ya Iringa kwa 12%.’’’’alisema Ayubu.

Kwa upande wake Afisa elimu wa mkoa Richard Mfugale alisema mwaka huu hakukuwa na tuhuma zozote za udanganyifu wa mitihani kama ilivyotokea miaka ya nyuma.

Mfugale alisema kuwa wanafunzi 413 hawakuweza kufanya mtihani kwa sababu mbalimbali ikiwemo utoro, vifo, ugonwa , mimba na kuhama.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Stevin Mhapa alisema wamefanikiwa kuongeza kiwango cha ufaulu kutokana na kufuata ushauri uliotolewa kwenye kikao kama hicho kilichopita sambamba na kufanya tathimini za mara kwa mara.

0 maoni:

Chapisha Maoni