Jumanne, 8 Novemba 2016

Wajasiriliamali zaidi ya 12,000 nchini kunufaika na elimu ya ujasiriamali ya TBL

Posted by Esta Malibiche on Nov 8,2016 in BIASHARA

 2

1
Meneja wa Uendelezaji Masoko wa TBL,Malaki Sitaki akizungumza
4
Baadhi ya wajasiriamali waliomaliza mafunzo ya RDP wilayani Bagamoyo katika picha ya pamoja
2
Baadhi ya wajasiriamali waliomaliza mafunzo ya RDP wilayani Ilala katika picha ya pamoja 3
Wajasiriamali waliomaliza mafunzo ya RDP wilayani Bagamoyo wakifurahi katika hafla ya kuwapongeza hivi karibuni
…………………………………………………………………………….
-Idadi yao kubwa ni wanawake
Kampuni ya TBL  inaendelea kutekeleza mpango wa kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wateja wanaouza bidhaa zake kupitia mpango wa Retail Development Programme ulioanza mwaka jana unaoenda sambamba na elimu ya Unywaji Kistaarabu.
Meneja wa Uendelezaji Mauzo wa TBL,Bw. Malaki Sitaki, amesema kuwa kwa kipindi cha muda mfupi yamepatikana mafanikio makubwa kutokana na mwitikio mkubwa wa wanaohitaji kupatiwa mafunzo ambapo kwa kipindi cha miaka 2 tayari mafunzo yamewafikia wajasiriamali zaidi ya  2,500 kutoka karibu mikoa yote nchini na matarajio ya kampuni ni kuwafikishia elimu zaidi ya wajasiriamali 20,000 hadi ifikapo mwaka 2019.
Mwitikio wa wahitaji wa mafunzo haya ni mkubwa na kinachofurahisha idadi kubwa ya wajasiriamali wanaoshiriki  mafunzo haya ni Wanawake.Hii kwetu ni faraja kubwa kwa kuwa tunaamini kuwaelimisha wanawake inakuwa umeelimisha jamii nzima na ni rahisi kuleta maendeleo na mabadiko endelevu kama ilivyo lengo la mpango huu”.Alisema Malaki
Alisema thatmini ya awali ya mpango imebainisha kuwa mafunzo yanaendelea  kuwanufaisha wasambazaji wa bidhaa za TBL ngazi ya chini (Retailer level) na asilimia kubwa ya waliopata mafunzo haya  wanaendelea kuendesha biashara zao na kujipatia faida inayowawezesha kuboresha maisha yao na familia zao  kwa kuzipatia lishe nzuri,watoto wao kupata huduma bora za kiafya na elimu .” Huu ndio mwelekeo wa uwekezaji wetu unaokwenda sambamba na kuleta mabadiliko kwenye jamii”.Alisema.
Mafunzo ambayo yametolewa kupitia mpango huu aliyataja kuwa ni mbinu mbalimbali za kufanya biashara kwa mafanikio,utunzaji wa mahesabu na kumbukumbu za mauzo,matumizi mazuri ya fedha,mipango ya biashara,sheria na miongozo ya biashara,huduma kwa wateja,elimu ya unywaji kistaarabu na utunzaji wa mazingira.
Suala la Unywaji wa Kistaarabu na mazingira tumeliweka kwenye mafunzo haya kwa ajili ya kuendeleza kampeni inayoendelea ya kuhakikisha jamii inatumia vinywaji kama viburudisho badala ya kulewa na kuleta athari kwa jamii ikiwemo kushindwa kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali ipasavyo.”Alisema Malaki.
Aliongeza kuwa TBL inatekeleza maazimio yaliyofikiwa na watendaji Wakuu wa makampuni yanayotengeneza vinywaji vyenye kilevi wakati wa kuadhimisha siku ya unywaji wa kistaarabu hivi karibuni ambapo waliazimia kujenga jamii zisizoathirika na ulevi katika maeneo yanapofanyia  biashara na kusambaza bidhaa zake.
Malaki alisema elimu ya Unywaji Kistaarabu itaendelea kutolewa katika jamii kupitia njia mbalimbali mojawapo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali kupitia Jeshi la Polisi kwa kusaidia katika kampeni za usalama barabarani kwa kuhamasisha madereva kutotumia vinywaji vyenye kilevi pindi waendeshapo vyombo vya moto.
Mwaka huu TBL ilikuwa mstari wa mbele kufanikisha Wiki ya Nenda kwa usalama barabarani ambapo ilishiriki katika uhamasishaji wa Usalama barabarani pia ilitoa huduma ya zahanati inayotembea ya ‘Zahanati Mwendo’ kwa ajili ya kupima afya za madereva na kutoa ushauri wa kiafya huduma ya aina yake nchini ambayo imewawezesha madereva wengi kupimwa afya zao na kupatiwa ushauri wa kitaalamu.

0 maoni:

Chapisha Maoni