Ujumbe kutoka kutoka jimbo la Eastern Cape kutoka nchini Afrika ya Kusini uko nchini kwa ajili ya kujifunza kutoka Tanzania namna bora ya fursa za kiuchumi kwa wanawake nchini, uwezeshaji wa wanawake na uendeshaji wa Benki ya Wanawake Nchini.
Akiongea na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga kiongozi wa Msafara wa ujumbe toka Afrika Kusini Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape, Mhe. Nancy Sihiwaji  amesema ziara yaoa inatokana na utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Wanawake Afrika uliofanyika Nchini Afrika ya Kusini kuhusu uwezeshaji wanawake kiuchumi.
Aidha ujumbe huu umetambelea Wizara hii ili kujifunza na kupata uzoefu kutoka Nchini ni kuona ni jinsi gani Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wameweza kuanzisha na kufungua Benki inayolenga kuwainua wanawake kiuchumi.
untitled-1Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Njinsia, Wazee na Watoto akiongea na wajumbe wa ujumbe wa jimbo la Eastern Cape hawapo pichani kutoka Afrika Kusini leo ofisini kwake.
untitled-2Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga alipomtembelea Wizarani kwake kwa leo katika ziara ya mafunzo ya siku moja kupata uzoefu wa uwezeshaji wanawake kiuchumi hapa nchini.
untitled-3Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape na ujumbe wake pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga  wote katikati wakiwa katika picha ya pamoja leo walipomtembelea kwa ziara ya mafunzo ya siku moja kupata uzoefu wa uwezeshaji wanawake kiuchumi hapa nchini.
untitled-4Mhe. Nancy Sihiwaji Mbunge wa Jimbo la Eastern Cape akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga zawadi ya skafu yenye ujumbe kutoka Jimbo la Eastern Cape leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Jinsia kutoka Wizara hiyo  Bw. Timoth Mgonja.(PICHA ZOTE NA ANTHONY ISHENGOMA)