Jumatano, 16 Novemba 2016

DKT MGWATU AAGIZA UPANUZI WA KARAKANA TEMESA RUKWA.

Posted by Esta Malibiche on Nov 16,2016 in TECHNOLOJIA

same2
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme – TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (kushoto) akizungumza na Meneja wa TEMESA Rukwa  Mhandisi Julius Ndosi (kulia), alipotembelea kituoni hapo.
same3
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme – TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (aliyesimama) akiongea na watumishi wa kituo cha TEMESA Rukwa alipotembelea kituo hicho hivi karibuni.
Picha zote na Theresia Mwami TEMESA Rukwa.
……………………………………………………………………
Na Theresia Mwami TEMESA Rukwa.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu amemuagiza Meneja wa TEMESA Rukwa Mhandisi Julius Ndosi kutumia eneo la karakana ya TEMESA Rukwa kupanua huduma zake badala ya kuwaachia watu binafsi kutoa huduma ambazo karakana hiyo ingeweza kuzitoa.
Dkt Mgwatu ametoa agizo hilo alipotembelea na kujionea utendaji kazi wa karakana ya TEMESA Rukwa na kusisitiza kuwa watendaji wa kituo hicho wanatakiwa maadili na uadilifu utekelezaji wa majukumu yao.
Ameongeza kuwa watendaji wa kituo hicho wanatakiwa kuwa wabunifu na kutumia rasilimali zilizopo kuongeza uwezo wa kutoa huduma zilizo bora na zinazozingatia viwango vya kimataifa.
“Nataka wewe kama Meneja wa kituo hiki uwe mbunifu kwa kutumia fursa zilizopo hapa Sumbawanga ili kuzalisha mapato zaidi” alisema Dkt. Mgwatu.
Aidha Dkt. Mgwatu ametoa miezi miwili kwa Meneja huyo kukamilisha na kuwasilisha mpango wa namna ya utekelezaji wa maagizo hayo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu yuko katika ziara ya kikazi katika vituo vya TEMESA Nyanda za Juu Kusini kutembelea na kukagua vituo hivyo ili kujionea changamoto mbalimbali pamoja na utendaji kazi wake.

0 maoni:

Chapisha Maoni