Ijumaa, 4 Novemba 2016

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA MAHOJIANO NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI IKULU LEO

Posted by Esta Malibiche on Nov4,2016 in NEWS

 t9

t11
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mtangazaji  Tido Mhando wakati akiuliza maswali  kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
t12
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Msanii Mrisho Mpoto akiimbwa wimbo wa “SIJONZE” wakati  alipokutana na wahariri  kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
t2 t3 t4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayoub Rioba wakati wa kupokea maswali kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
t5 t6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akijibu maswali 
kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
t7 t8 t9
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza mwanahabari Sammy Awami wa BBC wakati akiuliza maswali  kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
t10
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonazi wakati akiuliza maswali  kutoka kwa wahariri wa vyombo mbalimbali aliokutana nao kwa mahojiano leo Ijumaa Oktoba 4, 2016 katika ukumbi w3a mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam
………………………………………………………………………
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO-Dar es Salaam.
 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka waandishi wa habari nchini kutotumika kama mgongo kwa baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari katika kupinga muswada wa sheria wa huduma za habari wa mwaka 2016.
 
Aliyasema hayo leo Jijini Dar es Saalam wakati wa mkutano wake na Wahariri wa vyombo vya habari nchini katika kuhadhimisha mwaka mmoja wa Utawala wake, ambapo alisema kuwa kumekuwa na baadhi ya wamiliki wenye mashali binafsi katika kupinga mchakato mzima wa upatikanaji wa Sheria ya Huduma za Habari nchini.
 
“mchakato wa kupata Sheria ya huduma za habari umechelewa kutokana na sababu mbalimbali hivyo ninawataka wanahabari kutozungumza kwa mgongo wa wamiliki  mbalimbali wenye maslahi binafsi katika kupinga upatikanaji wa Sheria hiyo.
 
Alisema kuwa suala la Muswada wa Huduma za Habari upo mikononi mwa wabunge ikiwa ni muhimili unaojitegemea na hatoweza kuingilia maamuzi ya bunge na kuacha wabunge kutimiza wajibu wao katika utungaji na upatikanaji wa Sheria hiyo.
 
Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa anafahamu baadhi ya changamoto zilizopo kwa waandishi wa habari hasa katika masuala ya maslahi hivyo muswada huo utasaidia katika kutatua changamoto hizo na pia utaifanya tasnia ya habari kuwa taaluma itakayoheshimika kama taaluma nyingine.
 
Akizungumza kuhusu ushirikiano baina yake na vyombo vya habari, Rais Magufuli amewataka vyombo vya habari nchini kushirikiana, kusimamia uzalendo katika kulisukuma mbele gurudumu

0 maoni:

Chapisha Maoni