Posted by Esta Malibiche on Nov 7,2016 in MICHEZO
Lakini, wakati mchezo huo Na. 5
wa Kundi B, ukifanyika michezo mingine mitano ya raundi ya pili ikiwamo
mitatu ya Kundi A, imebidi iahirishwe na itapangiwa tarehe nyingine.
Sababu kubwa ya kuahirishwa kwa michezo hiyo ni uwingi wa wachezaji
kutoka timu zinazoshiriki ligi hiyo kujumuishwa kwenye timu ya taifa ya
Wanawake – Twiga Stars.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi
hiyo, michezo ya Kundi B iliyoahirishwa ni kati ya Majengo Women ya
Singida iliyokuwa icheza na Baobab ya Dpdoma kwenye Uwanja wa Namfua
mjini Singida wakati mechi nyingine ni kati ya Victoria Queens ya Kegera
iliyokuwa icheze na Sisters ya Kigoma – mchezo ulipangwa kufanyika
Uwanja wa Katiba mjini Bukoba.
Michezo ya Kundi A iliyoahirishwa
ni kati ya Fair Play ya Tanga iliyokuwa iikaribishe Mburahati Queens ya
Dar es Salaam kesho Novemba 8, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani ilihali
michezo mingine iliyoahirishwa ni ya Novemba 9, ambako JKT Queens ya Dar
es Salaam ilikuwa icheze na Viva Queens kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es
Salaam wakati Evergreen Queens na Mlandizi zilikuwa zitumie Uwanja wa
Karume, Ilala kucheza mechi yao hiyo.






0 maoni:
Chapisha Maoni