Jumapili, 6 Novemba 2016

DC KASESELA AKABIDHI MRADI WA MAJI KWA WANAKIJIJI LUPALAMA WENYE THAMANI YA MILL 35


Posted by Esta Malibiche on Nov 6,2016 in NEWS



Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akimtwisha Ndoo ya Maji Bi.Theobadina Ngailo Mara baada ya kukabidhi Mradi wa Maji katika kijiji cha Lupalama Jimbo la Kalenga uliogharimu kiasi cha Mill.35 na kufadhiliwa na Shirika la E.P.I.C (Everyday People Initiate Changes) la Marekani

Na Esta Malibiche
Iringa
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela amezindua mradi wa maji Saafi na salama katika kijiji cha Lupalama kilichopo katika Tarafa ya kalenga Wilayani Iringa,uliogharimu kiasi cha Tsh.35 Mill.

Mradi huo umefadhiliwa  na Shirika la E.P.I.C (Everyday People Initiate Changes) la Marekani liloanzishwa na Mwanamuziki wa Marekani Tinara Moore,ambaye aliwahi kutembelea Tanzania na baadae kuamua kutoa misaada mbalimbli.

Akikabidhi Mradi huo kwa wanakijiji wa lupalama mkuu wa wilaya ya Iringa amewaomba  wana kijiji hao kuusimamia vema mradi huo kwani Ofisi yake ina mpango wa kuhakikisha maji hayo yana sambazwa katika Maeneo Yote ya kijiji hicho ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa wingi.

‘’’’’’Matumaini  yangu kuona Maji haya yana wafikia wanakijiji wote wa lupalama ikibidi na maeneo ya Jirani wapate pia maji haya nitoe agizo kwa serikali ya kijiji kuunda kamati ya kusimamia na kutunza mradi huu ili uendelee kufanya kazi na kunufaisha wengi wakati mimi niki hangaika kuona jinsi gani tunapata pampu ya Umeme ikishindikana hata ya kutumia nguvu ya jua ili tusambaze maji haya sehemu nyingi zaidi”Alisema Kasesela

Katika hotuba yake Mkuu wa wilaya alihimiza wananchi kutumia vizuri chakula,kutokana na mvua kuchelewa kunyesha ili waweze kuepuka na baa la njaa,pia aliwasihi mara mvua zitakapoanza kunyesha wqatumie muda huo katika kilimo na wajitahidi kupanda mazao ya muda mfupiyatakayoweza kukomaa haraka na kuvunwa.

 Mvua mwaka huu sio za kuridhisha hivyo basi ipo hofu ya kukosekana chakula ni muhimu wananchi wakatunza chakula na kulima mazao yenye kuhimili ukamE’’’’’Alisema Kasesela

Aidha Dc Kasesela aliiagiza Serikali ya kijiji Kuanza mara moja Mchakato wa ujenzi wa kituo cha afya kijijini hapo kwani ni kero ya muda mrefu hasa kwa akina mama kwani wana lazimika kutembea kilomita saba kufuata huduma ya afya

 “Nawaombeni Zoezi hili  lianze mapema sana na ikibidi kila mwanakijiji ashiriki kukusanya mawe ya ujenzi na pindi mkiwa tayali ujenzi uanze mara moja”.Alisema Kasesela
Akizungumza wakati wa kukabidhi mradi huo Muwakilishi wa E.P.I.C Tanzania Bwana Johnson Mkini Kisinda alisema kuwa mradi huo umeghalimu pesa zaidi ya milioni therasini na tano hadi kukamilika .

‘’’’’ “Hiki ni kisima cha pili kwa urefu katika visima vyote tulivyo chimba kwani Lengo lilikuwa kuchimba mita sabini tu ila tulikosa maji tukalazimika kuchimba mita mia moja na themanini kwenda chini hadi kuyafikia maji.
Kisinda aliwataka wanakijiji wa Lupalama kuwa walinzi wa miundo mbinu hiyo ya maji kwani ni kwa faida yao wenyewe.


Theobadina Ngailo  ni mwanakijiji mkazi wa Lupalama akizungumza kwa niaba ya wanakijiji alisema kuwa kwa muda mrefu walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya kutembea  umbali mrefu kutafuta maji,na kushindwa kufanya shughuli za maendeleo kwasababu ya maji,hivyo alilishukuru shirika la E.P.I.C kwa kutatua changamoto hiyo

 ‘’’’’’’Tulikuwa tukilazimika kutembea saa zima kufata maji mtoni nabado maji haya kuwa ya uhakika kwa maana kipindi cha kiangazi mto ulikuwa una kauka jambo lililopelekea kupata shida kubwa sana katika upatikanaji wa maji. Tulikuwa tunatumia hata maji ya kwenye vidimbwi ambayo sio salama kwa matumizi ya binadamu kwani muda mungine tulikuwa tukichangia maji hayo na mifugo jambo lilipolekea kulipuka kwa magonjwa kama kuhara”.” ‘’’’Alisema Theobadina

 

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akikata utepe katika uzinduzi wa Bomba la maji katika kijiji cha Lupalama kulia kwake ni  Johnson Kisinda mwakilishi  Shirika la E.P.I.C hapa Nchini Tanzania, Kushoto ni Diwania wa  kata ya Lupalama.


Wanakijiji wa Lupalama Wilaya ya Iringa wakisikiliza jambo kutoka kwa mkuu wa wilaya,katika makabidhiano ya mradi wa Maji

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akisisitiza jambo wakati wa kukabidhi mradi wa Maji
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongoza kukinga Maji ya Bomba  mara baada ya kukabidhi Mradi wa Maji kwa wananchi wa kijiji cha Lupalama




0 maoni:

Chapisha Maoni