by Esta Malibiche on July 5, 2016
| Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamuhuri Wilaiyum akiapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Iringa |
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah akiapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Iringa
Mkuu
wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amewaapishwa wakuu wa wilaya watatu wa mkoa wa Iringa
na kuwakabidhi Irani ya chama cha mapinduzi ccm ili kutekeleza mambo mabalimbali ikiwemo kupambana na njaa pamoja na migogoro ya
mbalimbali inayowakabili wananchi.
Walioapishwa jana ni Mkuu wa
Wilaya ya Iringa Richad Kasesela,Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri
William na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Abdallah.
Akizungumza mara baada ya
kuwaapisha wakuu hao, Mkuu huyo wa mkoawa Iringa alisema ni muhimu
viongozi hao wakatambua kuwa serikali ya awamu ya tano inadhamira ya dhati ya
kuwatumikia wananchi na kwamba wajibu wao ni kuhakikisha wanatekeleza majukumu
yao bila ya upendeleo wowote.
“Serikali ya awamu ya
tano indhamiraya dhati ya kutumikia wanchi,hivyo nanyi katika maeneo yenu ya
kazi mnapaswa kuhakikisha mtaskeelzsa majukumuyenukwakuzingatia
sheriakauninuna taratibu na katika utatuzowakero za watu pasiwa na neno
njoo keshoau wiki ijayo’alisema Masenza.
Pamojana
kuwatakakushughulikia migogoroya wanachi piaawataka viongozi hao kuhakikisha
wanaondoa tatizo la njaa kwenye maeneo yao huku akibainisha maeneo sugu kwa
njaa mkoani hapakuwa ni Tarafa ya Isimani wilayani Iringa na Tarafa ya
Mahenge wilayani Kilolo.
Agizo lingine walilopewa
viongozi hao wateule ni kushughulikia tatizo la watumishi hewa ambalo
tayari serikali ya mkoa imechukua hatua yakuwabaini.
Alisema mkoa huo umebiani
uwepo wa wafanyakazi hewa 169 ambao ni idadib mpya inayotofauriana na
idida aliyootoa awali ya wafanyakazi 23 hivyo kutaka viongozi hao kuwachukulia
hatua watumishi hao kwamjibu wa sheria pamoja na watumishi waliosababisha uwepo
wao.
Kwa upande wao wakuu wa
wilaya hao wakizungumza mara baada ya kuapishwa walisema wamepokea
maelekezonakwamba watayatekeleza kwa kamawalivyoelezwa na mkuu huyo wamkoa.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa
Richard Kasesela alisema amekwishatenga siku moja katika kila wiki kwaajili ya
kushughulikia migogorombalimbali katikaeneolakena kuwataka wanachikufika
ofisini kilasikuya Alhamisi kumweleza kero zao.
Naye Mkuu wa Wilaya ya
Mufindi Jamhuri William alisema atahakikisha anasiamia sualala elimu
katikawilaya yake na kuifanya wilaya hiyokwua miongoni mwa maeneo ya watu
walioelimika.
Kwa upande wake Mkuu wa
Wilaya ya Kilolo Asia Abdallah alisema atahakikisha wazazi wa Wilaya hiyo
wanawawapatia watoto wao vifaa muhimu vitakavyowafanya wasome na kwamba mzazi
atakayezembea atamchukulia hatua za kisheria.

















0 maoni:
Chapisha Maoni