Jumatano, 20 Julai 2016

Serikali yapongezwa kwa kuwajali watu wenye mahitaji maalum

Postedy by Esta Malibiche  on July 20, 2016 in JAMII with No comments

1Wakonta Kapunda : Msichana mwenye umri wa miaka (22) akitumia ulimi kuandika meseji kwenye simu yake ya Mkononi  wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Dada yake Bi. Judith Assenga.Binti huyo ameanza kutumia kiungo hicho katika kuandika baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutokana na ajali mbaya aliyoipata mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa wakati wa Mahafali ya Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe Mkoani Tanga.
2Msichana mwenye umri wa miaka (22) Bi. Wakonta Kapunda akifanya mahojiano maalum na mwandishi wa Radio ya Kimataifa ya Ufaransa (Rfi) wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Binti huyo anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.
3Judith Assenga(kushoto) dada yake na Wakonta Kapunda akimuelekeza jambo mdogo wake  wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wakonta anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.
4Mratibu wa Masuala ya Habari katika Kampeni ya kumsaidia Wakonta Bw. Joseph Kithama akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) namba ambazo wadau wanaweza kutumia kumchangia Binti huyo anayehitaji msaada ili apatae matibabu na kutimiza ndoto zake za kwasaidia wengine wenye matatizo kama yake leo jijini Dar es Salaam.
5Kutoka kulia ni Wakonta Kapunda, Judith Assenga(dada yake na Wakonta), Mwajuma Selkemani na Chritina Rubangula(waliokuwa wanafunzi wenzake na Wakonta) wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Wakonta anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.

0 maoni:

Chapisha Maoni