Alhamisi, 21 Julai 2016

MWENYEKITI WA CCM DK. JAKAYA KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU DODOMA LEO


1Rais Dk. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Mh. Dk. Jakaya Kikwete wakati akifungua kikao cha Kamati Kuu ya ya Halmashauri kuu ya  CCM kilichofanyika leo Makao Mkuu ya CCM Dodoma kupendekeza jina la Mwenyekiti mpya wa CCM ambapo jina hilo litapelekwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa kwa ajili kupelekwa kwenye mkutano mkuu   na kuthibitishwa katika Mkutano Mkuu maalum wa CCM unaotarajiwa kufanyika Julai 23 mwaka huu mjini Dodoma, Katikati ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
2Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Mh. Dk. Jakaya Kikwete  akifungua kikao cha Kamati Kuu ya ya Halmashauri kuu ya  CCM kilichofanyika leo Makao Mkuu ya CCM Dodoma Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula na katikati ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurrahman Kinana.
3Rais Dk John Pombe Magufuli kushoto pamoja na Mwenyekiti wa CCM Dk Jakaya Kikwete na viongozi wengine wakiimba wimbo maalum wa CCM wakati mkutano huo uliofanyika leo Makao Mkuu ya CCM Dodoma
4
Mjumbe wa Kamati Kuu Ndugu William Lukuvi akizungumza na wajumbe wenzake Adam Kimbisa kushoto na Nape Nnauye Katibu Mwenezi wa CCM Taifa.
5
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM  Adam Kimbisa akuzungumza na wajumbe wenzake kutoka kushoto ni Nape Nnauye Katibu Mwenyezi wa CCM Taifa, Mama Zakia Megji , William  Lukuvi na Mohamed Seif Khatib.
6
Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akisalimiana na Wajumbe wa kamati kuu wakati alipowasili kuhudhuria katika mkutano huo.
7
Wajumbe wa Kamati Kuu Mzee Steven Wasira kulia na Msemaji wa CCM Christopher Ole Sendeka wakifurahia jambo kabla ya mkutano huo kuanza.
8Mjumbe wa Kamati kuu kutoka Zanzibar Sadifa Juma Khamis akizungumza na mjumbe mwenzake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Ndugu Abdallah Bulembo kutoka kulia ni Jerry Silaa na Hussein Mwinyi.

0 maoni:

Chapisha Maoni