Jumatano, 20 Julai 2016

SELEMAN JAFO ABARIKI MCHAKATO WA KUIGAWA HALMASHAURI YA KILOLO MKOANI IRINGA

Postedy by Esta Malibiche on July 20News

Naibu waziri wa  Nchi ofisi ya Rais Tamisemi Seleman Jafo akizungumza na Watumishi  wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo

NaibuWaziri Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kilolo


Watumishi wa Halmashauri ya Kilolo wakimsikiliza kwa makini Naibu waziri
  
Naibu waziri akikagua vyumba vya bweni la wavulana shule ya sekondari Kilolo





Waziri akiwa katika zahanati ya kituo cha Afya kilolo
 Picha na Esta Malibiche KALI YA HABARI BLOG]

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Seleman Jafo amebariki mchakato wa Wilaya ya Kilolo wa kutaka kuigawa Halmashauri hiyo  kuwa Halmashauri mbili.
Kwa sasa halmashauri hiyo imezaa mji mdogo wa Ilula ambao kwa sasa unapiganiwa na serikali ya mkoa pamoja na wadau mbalimbali kufikia hadhi ya kwua Halmashauri.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kaatika kijiji cha Nyanzwa katika mji wa Ilula Jafo alikokwenda kutembelea mradi wa kilimo cha umwagiliaji alisema kutokana na jiogorafia ya Wilaya hiyo wazo la kuugawa mji huo ni wazao sahihi.
 
Mchakato wa kutaka Halmashauri ya Kilolo kugawanywa uliibuka miaka mitatu iliyopita na tayari vikao mbalimbali vikiwamo ile vua ushauri vya Wilaya (DCC)na Mkoa (RCC)vimepitisha pendekezo hilo na kuliwasilisha ofisi ya Tamisemi yenye jukumu la kufikia uamuzi.
 
“Ofisi yangu imepokea maombi ya kutaka kugawanywa kwa Halmashauri ya kilolo,na tayari mda si mrefu wataalamu wangu watakuja kwa lengo la kukagua na kuona kama unakidhi sifa za kugawanywa”alisema Jafo na kuongeza:
“Lakini niseme hata wataalamu wakija na kutoa mapendekezo tofauti kuwa mji haujafikia hadhi hiyo ama ya bado mdogo mimi mwenyewe nitasema mbona nimefika huku na kujionea halihalisi”alisema.
Alisema kwa halihalisi ya jiografia ya Wilaya hiyo ni dhahiri inawawi vigumu watu wa upande wa Ilula kwenda kufuata huduma za kiutawala umbali wa zaidi ya KM 100 yalipo makao makuu ya Wilaya na Halmashauri ya wilaya hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Abdallah alisema ofisi yake imejipanga kuhakikisha inatekeelza maelekezo yote yanayotolewa na serikali kuu ili kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo.
“Mheshimiwa Naibu Waziri sisi tumejipanga vizuri na tunakuhakikishia tupo pamoja na tupo tayari kutekeleza maelezo yote kutoka serikali kuu kwa ajili ya kuwaletea wakazi wa Kilolo maendeleo.
Mbunge wa Jimbo hilo Venance Mwamoto alisema kutimizwa kwa ahadi ya kuigawa Halmashauri ya Kilolo kutasaidia wananchi kufikiwa na Huduma muhimu za kijamii.
 

0 maoni:

Chapisha Maoni