Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (Pichani juu kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa masuala ya Kidiplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani alipotembelea Wizarani kwa ajili ya kujitambulisha na kueleza nia ya Taasisi hiyo ya kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika miradi ya maendeleo hususan katika sekta ya elimu na afya.
Aga Khan 1
Sehemu ya wageni walioambatana na Balozi Lalani (hayupo pichani). Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Aga Khan nchini, Bw. Amin Kurji nao wakisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Muombwa na Balozi Lalani (hawapo pichani).
Aga Khan 2
Balozi Lalani naye akizungumza na Balozi Mwinyi alipotembelea Wizarani.
Aga Khan 3
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Ramla Khamis (kushoto), pamoja na Afisa Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Hellen Mgeta wakifuatilia mazungumzo.
Aga Khan 4
Mazungumzo yakiendelea.
Aga Khan 5
Balozi Mwinyi akiagana na  Balozi Lalani na Bw. Kurji  mara baada ya kumaliza mazungumzo.