Jumatatu, 18 Julai 2016

ALEX MSAMA ampongeza Waziri wa Habari NAPE NNAUYE kwa Kuwatetea Wasanii

Postedy by Esta Malibiche on july 18

Waziri wa Habari Nape Nnauye akiteta Jambo na Muigizaji Mkongwe hapa nchini King Majuto. 
1

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Action Mart Bwana Alex Msama akionyesha Stika za TRA zinazodaiwa kutolewa kimyemela na Baadhi ya watumishi wa TRA wasio waaminifu kwa kushirikiana na watu wanaodurufu kazi za wasanii kinyemela ili kujipatia kipato.

Kutokana na hali hiyo Msama Amempongeza Waziri wa Habari , Uramaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye kwa kazi aliyoifanya kutoka ofisini na kuenda kwenye maduka mbalimbali Kariakoo kwa ajili ya kusaka wezi wa kazi feki za wasanii.

Amesema Jambo hilo limemtia moyo kama mpigania haki wa kazi za wasanii ambaye amekuwa akipambana kila siku ili wasanii waweze kufaidika na jasho lao na ataendelea na kazi ya kuhakikisha wezi wote wa kazi za sanaa wanashughulikiwa kisheria na kuwafanya wasanii nao wanafaidi jasho lao.

2

Bwana Alex Msama akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam.

3

Bwana Alex Msama akionyesha baadhi ya stika za TRA zinazodaiwa kuibiwa na kugawiwa kinyemela kwa wauzaji wa Kazi feki za wasanii.

4

Hii ni moja ya CD feki iliyobandikwa stika za TRA.

5

Bwana Alex Msama akionyesha CD Feki na Stika zinazodaiwa kutuolewa kinyemela na baadhi ya watumishi wa wasio waaminifu.

0 maoni:

Chapisha Maoni