Jumatano, 20 Julai 2016

Prof. Ndalichako akiomba chuo Kikuu Ardhi kubuni majengo ya shule.

nda1Waziri wa Elimu , Sayansi , teknolojia na mafunzo ya  Ufundi Prof. Joyce Ndalichako wa kwanza kulia akitoa maelekezo kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi Prof. Idrissa Mshoro wa pili kulia alipotembelea banda la chuo hiko wakati wa ufunguzi wa wa maonesho ya 11 ya elimu ya juu , sayansi na teknolojia leo jijini Dar es salaam wa (tatu kulia) ni Katibu Mtendaji (TCU) Prof. Eleuther Mwageni.
nda2Afisa uhusiano Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Ardhi  Bi. Hadija Maulid wa kwanza kulia  akitoa maelekezo kwa baadhi ya wateja waliofika kwenye banda lao wakati wa ufunguzi  wa maonesho ya 11 ya elimu ya juu , sayansi na teknolojia yaliyofanyika jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………..
Na Ally Daud-Maelezo
Chuo Kikuu Ardhi kimetakiwa kubuni majengo ya shule kwa kiwango kikubwa na teknolojia ya sasa ili kuweza kupata majengo imara na usanifu mkubwa nchini kwa ajili ya maendeleo ya elimu kwa wasomi wa ndani.
Akizungumza hayo Waziri wa Elimu , Sayansi , teknolojia na mafunzo ya  Ufundi Prof. Joyce Ndalichako wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 11 ya elimu ya juu , sayansi na teknolojia  na kutembelea banda la chuo hiko amesema kuwa wana uwezo wa kubuni majengo hivyo wajitahidi na kuwakilisha kwake.
“Kwa kuwa mmeweza kunionyesha baadhi ya ubunifu wa majengo katika banda lenu basi nawaomba muendelee na kubuni majengo ya shule kwa usanifu mkubwa ili yatusaidie kukuza elimu nchini” aliongeza Prof. Ndalichako.
Katika maonyesho hayo yalioanza leo na kufikia tamati Julai 22 mwaka huu banda la Chuo kikuu Ardhi kina baadhi ya michoro ya majengo yaliyobuniwa na wanafunzi wa chuo hiko na ramani mbalimbali za majengo.

0 maoni:

Chapisha Maoni