Mkurugenzi
wa ufundi wa TBL Group, Gavin Van Wijk akiongea na waandishi wa habari
na wafanyakazi wa TBL Mwanza wakati wa hafla a kukabidhi tuzo
Meneja Msaidizi wa TBL Mwanza,Gabriel Pitso,akipokea tuzo kutoka kwa Mkurugenzi wa ufundi Gavin Van Wijk
………………………………………………………………………………………………………………………..
Kiwanda cha TBL Mwanza kilichopo
chini ya TBL Group na kikiwa moja ya kiwanda kinachoshikilia rekodi ya
ubora katika viwanda vya SABMiller duniani kimeshinda tuzo kubwa ya
Mackay kutokana na kufanya uzalishaji kwa kutumia pumba za mpunga.
Mackay ni tuzo kubwa ya SABMiller
ya kumuenzi mmoja wa Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Graham Mackay
ambaye katika kipindi chake cha kuitumikia kampuni hiyo aliendeleza kwa
kiasi kikubwa na alifariki miaka mitatu iliyopita ambapo kampuni
imeanzisha tuzo yake kwa viwanda vyake ambavyo vinafanya uzalishaji
unaoendana sambamba na malengo ya kampuni .
Malengo ya SABMiller ambayo
baadhi yake yanashahabiana na malengo ya Umoja wa Mataifa yamelenga
katika kufanya uzalishaji usio na athari kwa mazingira na unaoleta
mabadiliko kwa jamii kwa kuziwezesha kujikwamua kimapato.
Akiongea baada ya kukabidhi tuzo
hiyo kwa uongozi na wafanyakazi wa TBL Mwanza,Mkurugenzi wa Ufundi wa
TBL Group, Gavin Van Wijk,amekipongeza kiwanda kwa kuendelea kungaa na
kujinyakulia tuzo mbalimbali kama hii ya Mackay.“Ushindani ulikuwa
mkubwa na ulihusisha viwanda mbalimbali lakini hatimaye mmefanikiwa
kunyakua tuzo hii na kuweka rekodi ya kuwa kiwanda cha kwanza kuipata
barani Afrika”.Alisema
Alitoa shukrani kwa wateja wote
wanaoendelea kuiunga mkono kampuni kwa kununua bidhaa zake na kuongeza
kuwa siku zote kampuni itahakikisha inaongeza uzalishaji na kuingiza
bidhaa bora sokoni ikiwemo kusaidia huduma mbalimbali zinazoleta
mabadiliko kwenye jamii.
Akiongea juu ya tuzo hii katika
hafla ya kuipokea iliyofanyika kiwandani Mwanza ,Meneja wa kiwanda hicho
Gabriel Pitso, alisema kuwa kiwanda hicho ndicho cha kwanza kupata tuzo
hii nchini na ushindi huu umetokana na kufanya uzalishaji unaozingatia
utunzaji wa mazingira kwa kutumia mashine zinazotumia pumba za mpunga na
mashudu ambao kitaalamu hujulikana kama Dry –De- Husking (DDH) .
Alisema kampuni mama ya SABMiller
ilifanya utafiti na baada ya utafiti huo iliamua kabla ya kuanzisha
teknolojia ya uzalishaji usiotumia mafuta ya dizeli kwenye viwanda
vyake vyote ianzie katika kiwanda cha Mwanza ambapo katika miaka ya
kwanza ya majaribio mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na kutumia
teknolojia hii ikiwemo kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza
uharibifu wa mazingira.
Mbali na kupunguza athari za
uharibifu wa mazingira na gharama za uendeshaji teknolojia hii kwa kiasi
kikubwa inasaidia kuongeza vipato kwa wakulima wa pamba na mchele na
wafanyabiashara wanaokusanya pumba kwa ajili ya kukiuzia kiwanda “Zamani
pumba za mchele zilikuwa takataka lakini hivi sasa zimegeuka lulu kwa
kuwa zina soko tunazitumia katika uzalishaji hivyo kuna wafanyabiashara
wanapita maeneo mbalimbali wakizikusanya kwa ajili ya kutuuzia na huu
ndio uwekezaji mzuri unaonufaisha jamii inayoishi jirani na maeneo ya
kiwanda na ni moja ya malengo yetu”.Alisema.
0 maoni:
Chapisha Maoni