Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi leo mchana ametembelea Rais
mstaafu wa awamu ya pili Mh. Mzee Ali Hassan Mwinyi nyumbani kwake
Mikocheni jijini Dar es salaam.
Akiwa
nyumbani kwa Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais mstaafu na Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni walizungumzia mambo mbalimbali yahusuyo maendeleo ya Kinondoni
na historia ya nchi kwa ujumla. Rais mstaafu alimshukuru Mkuu wa Wilaya
ya Kinondoni kwa uamuzi wake wa kumtembelea na kumtakia kheri katika
majukumu yake.
Aidha mh. Mkuu wa Wilaya alimshukuru Rais mstaafu Mh. Ali Hassan Mwinyi na kumtakia afya njema na maisha marefu.
Aidha mh. Mkuu wa Wilaya alimshukuru Rais mstaafu Mh. Ali Hassan Mwinyi na kumtakia afya njema na maisha marefu.
0 maoni:
Chapisha Maoni