Ijumaa, 10 Juni 2016

DC HAPI AMTEMBELEA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI NYUMBANI KWAKE

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi leo mchana ametembelea Rais mstaafu wa awamu ya pili Mh. Mzee Ali Hassan Mwinyi nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es salaam.
Akiwa nyumbani kwa Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais mstaafu na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni walizungumzia mambo mbalimbali yahusuyo maendeleo ya Kinondoni na historia ya nchi kwa ujumla. Rais mstaafu alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni  kwa uamuzi wake wa kumtembelea na kumtakia kheri katika majukumu yake.
Aidha mh. Mkuu wa Wilaya alimshukuru Rais mstaafu Mh. Ali Hassan Mwinyi na kumtakia afya njema na maisha marefu.

0 maoni:

Chapisha Maoni