Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI ameziagiza Halmashauri za wilaya, Miji, Majiji pamoja na Manispaa nchini kuhakikisha majengo ya Halmashauri zao yanakuwa na hati miliki ili kuondoa migogoro kati yao na wananchi wenye tabia ya kuvamia maeneo kwa visingizio ni mali ya familia zao.
Waziri  Jaffu alitoa agizo hilo katika Mji mdogo wa Nduguti,wilayani Mkalama wakati wa kutembelea na kukagua majengo ya ofisi za Mkuu wa wilaya pamoja na majngo ya ofisi za makao makuu ya Halmashauri ya wilaya ya Mkalama.
Aidha Waziri Jaffu alisema kwenye maeneo mengi alikofanya ziara zake alibaini kwamba Halmashauri nyingi hazina hati miliki,jambo ambalo linaloweza kusababisha wajanja wachache kutokea na kutengeneza hati bandia za kuhalalisha maeneo hayo kwamba yalikuwa mali za babu zao.
“Hapa nimeshalizungumza pale nilipofika nimeambiwa hapa kuna takribani mita sguare hamsini ambao ukiugaanya kwa 4,060 kwa karibu sguare mita moja unazungumzia takribani ekari 12”alifafanua Jaffu.
“Ekari 12 na nikatoa maagizo kwamba katika sehemu mbali mbali zilizopita Halmashauri nyingi hazina hati miliki na mwisho wa siku ni kwamba watatokea wajanja watadai kwamba yale majengo ya serikali ni maeneo ya babu zao na inawezekana watu wakaja na suala zima la kuchonga hata hati feki hapo baadaye”alisisitiza Naibu waziri huyo.
Kwa hali hiyo kutokana na hofu hiyo Jaffu alitumia fursa ya ziara hiyo ya wilayani Mkalama kuziagiza Halmashauri zote ziwe na hati miliki za majengo yao.
Naibu waziri huyo alikwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa siyo hati miliki za majengo ya Halmashauri hizo peke yake bali akasisitiza pia ni vyema pia taasisi za serikali vikiwemo vituo vya afya pamoja na shule za msingi na sekondari zilizopo kwenye maeneo yao.
Hata hivyo Jaffu ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kibaha alibainisha kwamba kutokana na majengo hayo kutokuwa na hati miliki,kumechangia baadhi ya shule za msingi na hata sekondari kuanza kuvamiwa na wananchi kutokana na kile walichodai kuwa ni maeneo ya kwao na hata viwanja vya michezo kukosekana.
“Manake watu wamevamia kutokana na kutokuwa na hati miliki,kwa hiyo nilikuagiza  afisa ardhi kwamba hakikisha kwamba ajira yako ya kwanza kuwe na hati miliki ya jengo hili”alibainisha Naibu waziri huyo.
Akisoma taarifa ya ujenzi wa majengo ya utawala ya Halmashauri hiyo,Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama,Ramadhani Mohamedi alisema ujenzi huo ulioanza mwanzoni mwa mwaka huu unatarajiwa kukamilika sept,mwaka huu na kuelezea changamoto zinazoukabili ujenzi huo.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2014/2015 Halmashauri hiyo ilitengewa jumla ya shilingi milioni 450 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Mkalama baada ya kuwa imepokea kiasi hicho kidogo cha fedha za mwaka 2013/2014.
Kwa mujibu wa Mhandisi huyo wa wilaya ujenzi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Mkalama kwa awamu ya hiyo ya kwanza unakadiriwa kutumia shilingi 758,180,798/= na hiyo ikiwa ni pamoja na kodi ya ongezeko ya thamani,(VAT) ambayo ni karibu shilingi milioni na kitu.
“Mh Naibu Waziri ujenzi wa jengo hili ulianza januari,21,2016 na tunatarajia kuwa utakamilika sept,21,mwaka huu kwa awamu hii ya kwanza kwa maana itatumia miezi minane”alifafanua zaidi.
Katika hatua nyingine,kufuatia agizo la Rais John Pombe Magufuli la kuhakikisha ifikapo juni,30,mwaka huu kila Halmashauri inaondokana na tatizo la wanafunzi kukaa chini Kaimu afisa elimu msingi wa wilaya hiyo,Nasibu Pangahela alisema Halmashauri hiyo ilikuwa na upungufu wa madawati 14,840 na mpaka sasa imekamilisha utengenezaji wa madawati hayo yote kwa hali hiyo hapatakuwa na mwanafunzi atakaykaa chini katika wilaya hiyo.
Wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani Mkalama,Naibu Waziri Jaffu ametembelea na kukagua majengo ya ofisi ya mkuu wa wilaya,majengo ya utawala ya Halmashauri ya wilaya, kupokea madawati,kutembelea barabara ya Msingi-Yulansoni hadi Iguguno yenye urefu wa kilomita 25.
DSCN0057Mbunge wa jimbo la Iramba mashariki,Bwana Allani Kiullah akipokea taarifa ya utengenezaji wa madawati kutoka kwa kaimu afisa elimu wa wilaya ya Mkalama,Bwana Nasinu Pangaahela.
DSCN0059Mbunge wa jimbo la Iramba mashariki,Bwana Allani Kiullah (wa kwanza kutoka kulia) akimkabidhi Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI,Bwana Selemani Jaffu madawati
DSCN0062Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI,Bwana Selamni Jaffu(wa pili kutoka kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mbigigi,Bwana Donatus Lazaro (Aliyevaa shati la kitenge) kwa niaba ya walimu wengine wa wilaya hiyo jumla ya madawati mia moja yaliyochongwa na Mbunge wa jimbo la Iramba mashariki,Bwana Allan Kiullah kwa fedha za mfuko wa jimbo.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)