Jumatano, 29 Juni 2016

ASILIMIA 51 YA WATOTO MKOANI IRINGA NI WADUMAVU KUTOKANA NA UKOSEFU WA LISHE BORA



Kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa  ambae ni mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka Maafisa lishe mkoani hapa kuwasilisha taarifa ya lishe ya  chakula ya wananfunzi wa shule za msingi ofisini kwake kabla ya tarehe 30/6/2016
Akifungua  kikao cha wadau wa maendeleo  mkoa wa Iringa kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Iringa,mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela alisema  katika takwimu, mkoa unaongoza kwa udumavu  wa watoto  wenye umri chini ya miaka 5 hawana lishe.Halii hii inatokana na wazazi kuwa wazembe na kushindwa kuzinagtia  Elimu ya Afya inaypotolewa katika vituo vya afya.
Kasesela alisema mkoa wa Iringa ni miongoni mwa mikoa inayozalisha chakula kwa wingi ingawa bado unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa lishe kwa watoto na akina mama wajawazito hali inayopelekea udumavu.
Hali hiyo inatokana na wazazi kutokuwa karibu na watoto wao,kujikita zaidi katika shughuli za biashara na ulevi  na kushindwa kuzingatia Afya ya lishe kwa watoto.
‘’’Ingawa mkoa wetu unazalisha chakula kwa wingi lakini changamoto ya watoto kukosa lishe na kusababisha udumavu ni mkubwa.wazazi tunatakiwa tuzingatie Afya kwa watoto ili mka uweze kuondokana na hali ya udumavu kwa watoto.
Aidha Kasesela alisema hali ya madawati kwa mkoa wa Iringa karibu wilaya zote zimetekeleza na zinaendelea kutekeleza   ingawa changamoto ipo kwa watengenezaji lakini hadi tarehe 30/6/2016 kama agizo la Mh.Rais linavyosema yatakuwa yamekamilika ili  watoto watakaporejea shuleni wakute madawati yako tayari
Kwa upande wake Afisa lishe wa Mkoa wa Iringa Sizo Nzogere alisema  pamoja na mikoa ya Iringa na njombe  ni miongoni mwa mikao inayozalisha chakula kwa wingi ,lakini kuna tatizo la  kubwa la udumavu kutokana na hali ya lishe kuwa duni. Kila siku watoto 130  wanakufa pamoaja na akina mama 1600 kwa mwaka  wanakufa kutokana matatizo ya utapia mlo.hii inatokana na uwezo mdogo wa  kutozingatia umuhimu wa lishe.
Nzogere alisema mikakati iliyowekwa na mkoa ili kuhakikisha akina mama wajawazito wanazingatia swala la lishe ni pamoja na kuwajengea uwezo wahudumu wa afya ili waweze kutoa Elimu sahihi ya lishe katika vituo vya kutolea  huduma za afya.Kuendeshwa kwa kamati ya lishe katika Halmashauri zote zinazowahusisha viongozi wa dini kujadili mikakakti na changamoto mbalimbali za lishe ili kutokomeza hali ya udumavu kwa  katika mkoa.
Aidha alisema ili kuzuwia uatapia mlo katika mkika wa Iringa  Elimu inatakiwa itolewe kwa  wananchi ili mama mjamzito toka mimba inatungwa aweze kuzingatia  swala la lishe ili kumlinda motto wake akiwa tumboni hadi kuzaliwa.
 ‘’’’’’’’’’ Jumal ya vifaa 610 vya kupimia hali ya lishe kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano vimesambazwa   katika Halmashauri.Utoaji wa Elimu lishe,madini joto,ulaji unaofaa,viatamini A ,dawa za  minyoo,unyeshaji  ulishaji watoto wadogo na   wachanga na  inaendelea kutolewa  kwa wazazi /walezi  kila siku katika vituo 217 vinavyotoa huduma ya mama na motto ambapo hadi sasa walezi 129839 wamepokea Elimu lishe  katika kipindi cha januari,May’’’’’’’alisema…..
Pascal Nsana ni miongoni mwa wadau wa maendeleo waliohudhuria kiao hicho cjha wadau wa maendeleo  nae alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo katika lishe inatokana na wananchi kutokyua na Elimu tya kutosha kuhusu umuhimu wa kuzingatia lishe .
‘’’’Mkoa unachakula cha kutosha  namna ya kuandaa chakula na kuzingatia lishe  Elimuinatakiwa kutolewa juu ya makundi matono ya chakula yanayotakiwa kuzingatiwa mara mama anapokuwa mjamzito na baada ya kujifungua na jamii kwa ujumla’’’’’’alisema


0 maoni:

Chapisha Maoni