Alhamisi, 30 Juni 2016

WAFANYAKAZI WA ABANA WAANDAMANA KUDAI MIL 400 WANAZODAI

ma1Wafanyakazi wa kiwanda cha kuchapisha vitabu cha ABANA Printers ltd,kilichopo kata ya Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani,wakiandamana kudai mishahara na mafao yao wanayodai kwa kipindi cha miaka miwili na nusu ambayo yamefikia mil 400 .
(Picha na Mwamvua Mwinyi) 
———————————————————–
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
WAFANYAKAZI wa kiwanda cha uchapishaji vitabu(ABANA Printers Ltd) kilichopo kata ya Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ,wanadai fedha za mishahara na mafao yao kiasi cha sh.mil.400 tangu mwaka 2014 bila mafanikio.
Aidha wafanyakazi hao waiomba serikali ya awamu ya tano kuingilia kati tatizo hilo kwani wameshapigania haki zao kupitia mahakamani ,wizara,idara na vyama vinavyojishughulisha kutetea haki za wafanyakazi lakini hakuna msaada walioupata.
Wameeleza kuwa hadi sasa wanaishi katika maisha magumu  huku wengine wakiwa wamefukuzwa kwenye nyumba walizopanga  na wenzao watatu wamefariki kutokana na ugonjwa wa moyo.
Hayo yamejiri jana baada ya wafanyakazi hao kuchukua hatua ya kufanya maandamano nje ya kiwanda hicho na kisha kumfikishia kilio chao mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi (CCM)Bagamoyo,alhaj Abdul Sharif ili aweze kuwasaidia kulipwa haki zao.
Mwenyekiti wa tawi la chama cha wafanyakazi tawi la ABANA printers Wilbard Ikigo ,alidai kuwa mmiliki wa kampuni hiyo anajigamba kwa kusema serikali ipo mkononi mwake hivyo hawezi kuchukuliwa hatua yoyote.
Alisema ni miaka miwili na nusu sasa tangu watelekezwe na mwajiri wao hali iliyosababisha kuingia katika mgogoro na mmiliki huyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni