Mabaki yanayokisiwa kuwa ya ndege ya Malaysia yapatikana TZ
Hilo litawezekana tu wakati watengenezaji wa ndege hiyo watafika na kuchunguza mabaki hayo.
Shirika la habari nchini Malaysia Bernama lilimnukuu waziri uchukuzi nchini humo Liow Tiong Lai, akisema kuwa mabaki ya ndege hiyo yatafanyiwa uchunguzi kubainia ikiwa yana uhusiano na ndege ya Malaysia iliyopotea ya MH370.
Ndege hiyo ya Boeing 777 nambari MH370 ilitoweka 2014 ikiwa na watu 239 muda mfupi baada ya kupaa kutoka Kuala Lumpur ikielekea Beijing.
Hivi majuzi, mabaki ya ndege sawa na hiyo yalipatikana Madagascar lakini baada ya uchunguzi ikabainishwa kwamba hayakuwa ya ndege hiyo ya MH370.
0 maoni:
Chapisha Maoni