Jumapili, 26 Juni 2016

ZULMIRA ATAKA KAZI KWA PAMOJA KUHAMI MAENEO YA URITHI WA DUNIA

Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues amewakumbusha wadau wa urithi wa dunia na maeneo ya hifadhi kufanyakazi kwa pamoja kwa lengo la kuhifadhi na kuyaendeleza maeneo hayo bila kuondoa ushiriki wa wananchi wanayozunguka.
 
Kauli hiyo ameitoa katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia mjini Marangu Moshi, kufuatia makubaliano na serikali ya Tanzania.
 
Alisema akizungumza na washiriki kwamba UNESCO inachofanya ni kuanzisha safari ambayo inaweza kuwa ngumu na ndefu lakini washiriki wake ni lazima kutambua namna ya kuendelea kufanya menejimenti ya maeneo ya hifadhi na urithi wa dunia kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
 
Akifungua mafunzo hayo ambayo wataalamu ni washiriki wenyewe wakitumia njia ya kuelewa ya methodolojia ya uchambuzi wa vikwazo (Bottleneck Analysis Methodology) alisema safari ya kufanikisha menejimenti ya maeneo hayo duniani na hasa hapa nchini ni yenye changamoto nyingi na kwamba wadau wote wanatakiwa kuwa pamoja kuvishinda vikwazo hivyo na kuifanikisha safari.
 
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza katika warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
 
(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
 —————————————
Akizungumza katika warsha hiyo ambayo imechukua wadau mbalimbali wa masuala ya urithi na menejimenti zake kutoka serikalini, taasisi zisizo za kiserikali na wananchi wengine, alisema kwamba maeneo hayo yamezungukwa na wananchi na pamoja na kuwawekea sheria za kutoharibu na kuyachakaza ipo haja ya kushirikiana nao namna ya kupanga kuyaendeleza maeneo hayo huku yakiwa yamebaki katika hali inayotakiwa.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kupanga maendeleo katika maeneo ambayo ni ya urithi wa dunia, binadamu na maeneo ambayo uhai unaweza kuwepo.
Aidha akifafanua zaidi mtawala huyo wa UNESCO nchini Tanzania amesema mafunzo hayo yamelenga kuwapa wahusika nadharia zinazofaa katika safari ndefu ambayo UNESCO nayo itashiriki na isingelipenda kumwacha hata mtu mmoja nyuma.
Mafunzo hayo yanatolewa kufuatia mpango wa UNESCO wa kutaka kuwa na uhakika na kuhami maeneo hayo ya urithi; huku mamlaka zikitoa ushirikiano ili kuwezesha malengo ya maendeleo endelevu, ambayo ndiyo ajenda ya dunia kuelekea 2030, yanafikiwa bila kuathiri maeneo tajwa.
Ofisa anayeshughulikia watu na maeneo yenye uhakika wa uhai: Biashara zinazozingatia mazingira na uchumi unaombatana nao kutoka Sekta ya Sayansi Ofisi ya Unesco, Dar es salaam, Myoung Su Ko akiwasilisha mada kwa washiriki wa warsha hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Resort mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
 
Alisema kwa kuwa kitaifa, serikali imeshatoa matamko ya kisera na kuweka mikakati ya utekelezaji wa taratibu za kuhami maeneo ya kiutamaduni na ya asili ipo haja ya wadau wengine kuona namna ya kufanyakazi kama timu katika safari ambayo kila mmoja anastahili kuwaijibika kwa namna yake hata kama kunatokea changamoto.
Alisema wadau wanatakiwa kuangalia namna ya safari zao zinavyostahili kufanywa na kuwa, kwa lengo la kutumia raslimali zilizopo kutekeleza mipango ya maendeleo na ya kuhami maeneo hayo bila kutegemea msaada wa wafadhili au wahisani.
Awali katika ujengaji wa wazo la mafunzo ilielezwa kuwa pamoja na kuwapo na juhudi kubwa za kuhami maeneo ya urithi wa dunia na kuyasajili maeneo ambayo uhai unaweza kuwapo na wanadamu, kumekuwepo na changamoto kubwa za maendeleo ambazo zinatishia kuvuruga mfumo tete wa ikolojia uliopo.
Katika kufanikisha hifadhi ya maeneo hayo kumeonekana changamoto za upungufu wa rasilimali watu wenye uwezo na vifaa vya kushughulikia uharibifu, ukosefu wa uwezo wa kuhifadhi maeneo hayo kwa kuoanisha na uwapo wa watu.
Mtaalamu wa programu na utamaduni kutoka Ofisi za Unesco Afrika Mashariki Bi. Karalyn Monteil akiwasilisha mada kuhusu makubaliano ya ulinzi katika maeneo ya urithi na utamaduni wa dunia katika warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa juma mjini Marangu, Moshi.
 
Continue reading →

0 maoni:

Chapisha Maoni