Na Lydia Churi- MAHAKAMA YA TANZANIA
Jaji Mkuu wa Mahakama ya
Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman leo amefanya ziara ili kukagua
miradi ya ujenzi wa Mahakama za Wilaya na Mwanzo zinazojengwa mjini
Kibaha na Kigamboni.
Aidha, katika ziara hiyo,
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Kattanga alimweleza Jaji
Mkuu kuwa Mahakama ya Tanzania imeamua kutumia Teknolojia ya kuongeza
ufanisi kwa ubora wa hali ya juu na gharama nafuu iitwayo Moladi.
Alisema kupitia Teknolojia
hiyo, jengo huweza kukamilika ndani ya siku 45 mpaka 70 huku ikiokoa
gharama za ujenzi kwa kati ya asilimia 40 na 45.
Alisema kutokana upungufu
mkubwa wa Mahakama nchini Mahakama ya Tanzania iliunda timu
iliyokishirikisha Chuo Kikuu cha Ardhi na Baraza la Ujenzi la Taifa
(National Construction Council) ili kutafiti teknolojia itakayotumia
muda mfupi na yenye gharama nafuu kujenga majengo ya Mahakama nchini.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa
Mahakama, ujenzi unaoendelea sasa katika maeneo ya Kibaha, Kigamboni,
Mkuranga, Bagamoyo, Kinyerezi, Kawe na Ilala ni sehemu ya utafiti wa
teknolojia hiyo ili baadaye itumike kwenye ujenzi wa mahakama nyingine
katika maeneo mbalimbali nchini.
Alisema Mahakama ina upungufu
wa majengo katika maeneo mbalimbali nchini ambapo kuna majengo 960 tu
wakati mahitaji ni kuwa na majengo 3963 katika kila kata nchini.
Aliongeza kuwa kupitia teknolojia hii mahakama itajenga majengo bora na
mengi kwa kipindi kifupi.
Moladi ni teknolojia
inayotumika kujenga nyumba bora kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu
iliyoanzishwa nchini Afrika ya Kusini mwaka 1986 ambapo ukuta unaojengwa
kwa kutumia teknolojia hii hukauka kwa siku moja ili kupisha hatua
nyingine ya ujenzi kuendelea.eknolojia hii mahakama itajenga majengo bora na mengi kwa kipindi kifupi.
Moladi ni teknolojia inayotumika kujenga nyumba bora kwa
muda mfupi na kwa gharama nafuu iliyoanzishwa nchini Afrika ya Kusini
mwaka 1986 ambapo ukuta unaojengwa kwa kutumia teknolojia hii hukauka
kwa siku moja ili kupisha hatua nyingine ya ujenzi kuendelea.
0 maoni:
Chapisha Maoni