Alhamisi, 30 Juni 2016

SERIKALI MKOANI IRINGA YATEKELEZA AGIZO LA MH.RAIS KWA ASILIMIA MIA MOJA


Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa  Amina Masenza  akitazama  madawati  yaliyokamilika kulia ni  afisa  habari wa Manispaa ya  Iringa  Sima Bingileki

Mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa  Amina Masenza  kulia  akimkabidhi  madawati 100  mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa Bw. Ahmed  Sawa   leo baada ya  mkoa kukamilisha utekelezaji wa agizo la Rais kuhusu madawati 
Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya  wilaya ya  Kilolo kulia  akipokea madawati  kutoka kwa  mkuu wa mkoa wa Iringa
Mwakilishi  wa mkurugenzi wa Halmashauri ya  Wilaya ya  Iringa Bi  Hawa akiwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Masenza mara  baada ya  kukabidhiwa madawati
Na Esta Malibiche.blogspot.com


Serikali mkoani Iringa imetekeleza agizo la Mh.Rais Dr.John Magufuli aliyowaagiza wakuu wa mkoa nchini,kuhakikisha ifikapo tarehe 30/6/2016 wawe wamekamilisha mawadati katika shule zenye uhaba.

Akikabidhi madawati kwa wakurugenzi wa wilaya mkoani hapa, Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema serikali yake imetengeneza madawati  21 ,304 kwa ajili ya shule za Msingi  na madawati  3,665  kwa ajili ya Shule za Sekondari.

Masenza aliongeza kuwa madawati 8,163 kwa ajili ya Shule za Masingi na mengine 1,264 kwa ajili ya Shule za Seondari bado yanatengenezwa katika karakana mbalimbali na kweamba pindi yatakapokamilika yatafanya mkoa huokuwa na ziadi ya madawati badala ya upungufu.

Alisema kuchelewa kukamilika kwawakati kwa kazi ya kutengenezamadawati katika katika Halmashauri mbalimbali mkoani hapa kulitokana na wakandarasi wanaotengenezaa madawati kuwa na kazinyingi.

Hata hivyo alifafanua kuwa Madawati yaliyobaki kwa Halmashauri za Manispaa ya Iringa,Kilolo,Mufindi,Wilaya ya Iringa yanatarajia kukamilika kati ya Julia 3 na 15 huku Halmashauri ya Mji wa Mafinga ikitarajia kukamilika Julia 20 mwaka huu.

“Kazi ya kutengeneza madawati itakapokamilika Shule za Mkoa wa Iringa hazitakuwa na upungufutena wa madawqati bali zitakuwa na ziadiyamadawati 850 na hiini kutokana na baadhi ya Halkmashauri kuwa kutengeneza madawati ya zaidi na mengine niyaleyaliyotolewakutoka Ofisi ya Mkoawa Iringa”alisema Masenza.
Masenza ambaye pia alitumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi na wadaumbalimbali wakiwamoawafanyakazi waliojitolea kuchangia madawatihayo alisema hadikazihiyoinakamilika jumla ya Sh 50.4milioni zimetumika kutengeneza madawati hayo.
“Nitumie fursa hii kuwashukuru wadau mbalimbali,wafanyakazi  wa Halmashauri na wananchi wote walioona umuhimu wa kuchangia upatikanaji wa madawati haya”alisema Masenza na kuongeza.
“Mchango wao umekuwa na umuhimu katika kuwaandaa vijana wetu tunapoelekea Taifa lauchumi wa kati ifikapo mwaka 2030,michango yao ndiyo iliyosababisha kuwapo kwa ziada hiyo,kwani mkoa umetoa madawati 200 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na madawati 100 kwa Halmashauri za Kilolo,Iringa,Mji Mafinga na Mufindi”alisema Masenza.


0 maoni:

Chapisha Maoni