K
Wananchi wa Mtaa wa Mwambisi wakifua kwa kutumia maji ya mabondeni
Wakazi wa Mtaa wa Mwambisi Kata ya Kongowe iliyopo wilayani wakichota
maji ya mabondeni kutokana na maji safi na salama katika kata hiyo
kutoka mara moja kwa wiki na kusababisha kero na hofu kwa watumiaji wa
maji hayo. Picha zote na Elisa Shunda
Wananchi wa mtaa huo wakielekea katika eneo la Bonde la Miti Mirefu
kuchota maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kama kufulia nguo,kupikia
na kunywa jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa afya yao.
NA ELISA SHUNDA,KIBAHA
Serikali imeombwa kuingilia kati suala
la ukosefu wa upatikanaji wa maji safi katika kata ya Kongowe eneo la
Mwambisi ambalo maji yamekuwa yakitoka mara moja kwa wiki na kusababisha
wananchi kutumia maji ya mabondeni yasiyo salama kwa matumizi ya
binadamu.
Wakizungumza na Raia Tanzania,jana
wakazi wa maeneo mbalimbali wa kata hiyo walisema kuwa kutokana na
kutopatikana kwa maji safi na salama kwa wakati timilifu imepelekea
watoto wananchi kuwa na mashaka na afya zao kwa kuhofia kupata magonjwa
mbalimbali kama kuhara,kuumwa matumbo na kichocho.
Akichangia hoja hiyo mkazi wa mtaa wa
Mwambisi,Maria Nicoulas alisema kuwa kutokupatikana kwa maji safi katika
eneo la mwambisi ni kero kubwa sana kwa akina mama ambao muda mwingi
wanautumia kusubiri maji mabondeni na pia maji yenyewe siyo salama kwa
matumizi ya nyumbani lakini pia inaweza ikagombanisha familia kati ya
baba na mama kwa kuingiza hisia tofauti kwa kuwa unaweza ukakaa kusubiri
uchote maji hata masaa matatu.
“Sisi akina mama tunapata shida sana
kupata maji kwa kuwa hata sehemu tunapoenda kuchota maji ni mbali na
nyumbani na pia maji yenyewe huko kwenye mabonde ya mpunga ni mbali
inachukua muda mwingi hadi kuludi nyumbani kwa hali kama hii inaweza
kusababisha ugomvi kati ya baba na mama kwa kuingiza suala la wivu wa
kimapenzi kumbe masikini ni kutokana na umbali wa sehemu tunapochota
maji na foleni iliyopo hivyo tunaiomba serikali iangalie kuhusu tatizo
hili”Alisema Maria
Mkazi wa Bamba, Juma Abdul,alisema kuwa
kutokana kukatika mara kwa mara kwa maji katika maeneo mbalimbali ya
kata hiyo imekuwa ni kero na usumbufu kwa wananchi ambapo huwaletea
kutumia fedha nyingine ya ziada kununua maji safi wakati mabomba yapo
lakini hayatoi maji.
Aidha wananchi hao wananchi hao
wameiomba serikali kutoa msaada wa hali na mali kuhakikisha huduma hiyo
muhimu inarejea kama hapo awali ili kuondoa uwezekano wa kutokea
milipuko ya magonjwa ya matumbo na kichocho.
Akichangia kuhusu kero hiyo Aliyekuwa
mgombea Udiwani wa kata hiyo kupitia Chama cha Wananchi (Cuf),Mathas
Kambi,alisema kuwa suala la maji safi na salama kwenye kata ya kongowe
ni tatizo sugu sana,linatokana na sababu kuu zifuatazo kwanza viongozi
wa kata pamoja na viongozi wa serikali za mitaa kutotambua ufuatiliaji
wa kero hiyo, pili dawasco wenyewe pia hawako sawa kwenye huduma zao,
kwa maana miundombinu yao kwenye usambazaji haipo sawa.
“bomba kubwa linaweza kuharibika visiga
wiki nzima watu wa kongowe tunaweza kukosa maji kutokana na tatizo hili
afadhali ya mwambisi na Bamba maeneo ya kwamwami upande wa kulia kama
unaenda mlandizi kule hawajui maji tokea kongowe imefahamika eneo la
bamba upande wa kushoto kuna watu wamechangishwa pesa na mwenyekiti wao
Mavala mamilion ya pesa mpaka leo maji hakuna ni utapeli mtupu , miembe
saba B toka imezaliwa mpaka leo hawajui lini watapata maji safi na
salama ,huko mwambisi ndiko tatizo kama linavyojionyesha”Alisema Kambi
Akizungumza kuhusu suala hilo Diwani wa
Kata ya Kongowe,Iddi Kanyalu,alisema kuwa tatizo hilo limefika ofisini
kwake na kusema kuna shida ya kukatika kwa maji sana katika eneo la
Mwambisi na Vikunai na ameshalipeleka katika ofisi za Shirika la
majisafi na majitaka Dar es salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha alisema
uongozi wa shirika hilo wamemuambia kuwa tatizo kubwa ni baadhi ya
wananchi wanajiunganishia mabomba kiholela na muda si mrefu wataanza
kufanya oparesheni katika makazi ya watu.
“Nimepata taarifa za kuwepo kwa shida ya
maji katika maeneo mbalimbali ya kata yangu ya Kongowe nimefikisha kwa
uongozi wa Dawasco ambapo wameniambia kutokea kwa hali ya kukatika maji
sababu kubwa ni baadhi ya wananchi ambao si waaminifu wamejiunganishia
mabomba kinyume na sheria hali inayosababisha ukosefu wa maji na pia
uongozi umeniambia kuanzia wiki hii wanaanza oparesheni ya kupitia
katika makazi ya watu ili kubaini watu waliojiunganishia maji
kiholela”Alisema Kanyalu
0 maoni:
Chapisha Maoni