Jumamosi, 21 Mei 2016

Serikali kuanzisha vituo vya ununuzi wa mazao ili kumlinda mkulima


Wakala wa Vipimo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa inakusudia kuanzisha  vituo maalum vya ununuzi wa mazao ya wakulima (buying centres) katika vitongoji nchi nzima ili kuondoa unyonyaji na ukandamizaji unaofanwa na wachuuzi wa mazao ya wakulima.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo Mhe. Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni lini Serikali itasimamia sheria kuondoa unyonyaji unaofanywa na wachuuzi wakati wa kununua mazao ya wakulima.
Alisema kuwa katika kutekeza hayo hakuna mfanyabiashara atakayeruhusiwa kusafirisha mazao ambayo yamefungashwa kinyume kinyume cha Sheria ya vipimo na kuongeza kuwa katika kusimamia jambo hilo vitaanzishwa vituo maalum vya ukaguzi bila kusabaisha usumbufu katika ufanyaji biashara.
Mhe. Mwijage amewaagiza Maafisa Ugani walioko vijijini watumike kusimamia matumizi ya vipimo rasmi katika vituo hivyo na kutoa taarifa zote muhimu kwa Wakala wa Vipimo.
Aidha ,alisema kuwa Serikali imeamua kufanyia mapitio Sheria ya Vipimo sura 340 ili kuondokana na unyonyaji na ukandamizaji unaofanywa na wachuuzi wa mazao ya wakulima.
Alisema kuwa Serikali imeamua kufanyia mapitio ya Sheria hiyo ili kuweka mazingira mazuri kwa lengo la kumlinda muuzaji kwa kuwadhibiti manunuzi wanaotumia njia za udandanyifu wakati wanaponunua mazao ya wakulima.
Mhe. Mwijage alisema kuwa katika kipindi kifupi kijacho Serikali itawalisha mabadiliko hayo bungeni ili ifanyiwe marekebisho yanayostahili.
Aidha , Waziri huyo alisema kuwa pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vipimo yanatarajia kufanywa , Wakala wa Vipimo imewasilisha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mapendekezo ya kutungwa kwa sheria ndogo(by laws)  ili ziweze kuwaongoza wakulima na wafanyabiashara kufungasha mazao.

0 maoni:

Chapisha Maoni