Jumanne, 31 Mei 2016

Kampuni ya Regency Innovation Solutions na United Bank for Africa [Tanzania] wazindua kadi ya malipo ya kipekee Afrika

1Bw.Tesha Philemon Kaimu Mkurugenzi wa KItengu cha Huduma za Kibenki Mtandaoni Benki ya UBA kushoto akibadilishana mikataba na Bw. Mike Raymond Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Regency Innovation Solutions baada ya kusaini mkataba wa kutoa huduma ya kadi ya malipo ya kipekee ya Visa inayoitwa  Mimosa Black Card leo kwenye hoteli ya Regency Park Mikocheni jijini Dar es salaam.
3Bw.Tesha Philemon Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Kibenki Mtandaoni Benki ya UBA kushoto na Bw. Mike Raymond Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Regency Innovation Solutionswakionyesha  kadi ya malipo ya kipekee ya Visa inayoitwa  Mimosa Black Card iliyozinduliwa leo baada ya kampuni hizo kutiliana sahihi mkataba wa kufanya biashara kwa pamoja.
4Bw.Tesha Philemon Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Kibenki Mtandaoni Benki ya UBABw.Takizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwenye hoteli ya Regency Park Mikocheni jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………………………………..
Kampuni ya uvumbuzi na suluhisho inayoitwa Regency Innovation Solutions na benki ya UBA ya Tanzania wamesaini mkataba wa maelewano wa kutoa huduma ya kadi ya malipo ya kipekee ya Visa katika bara zima la Afrika wakianzia nchini Tanzania. Taarifa hii imetolewa leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kadi mpya ya malipo itakayoitwa Mimosa Black Card, kadi ambayo itaruhusu mteja kuweka na kutoa fedha bila ya kuhitaji akaunti ya benki.
Mkurugenzi Mkuu wa Regency Innovation Solution Mike Raymond alisema “Tumefurahi kushirikiana na benki ya UBA Tanzania katika uendelezaji wa uvumbuzi ambao utaanzia hapa Tanzania. Lengo letu ni kuleta suluhisho zilizo salama na kuaminika kwa wateja wetu. Kadi hii ya Mimosa ni ya kisasa ambayo sio tu ni salama na inayorahisisha huduma bali ina huduma nyingine nyingi na zawadi kwa wateja. Kupitia huduma hii tunaongeza wigo wa huduma za kifedha katika nchii ya Tanzania haswa kwa sababu kadi hii imeunganisha na huduma za pesa kupitia mitandao ya simu.”
Kadi hii mpya ni sawa na kadi ya kawaida ya malipo ya kabla ila ni ya kipekee kwa sababu haiunganishwi na akaunti ya benki hivyo kuifanya kuwa ya gharama nafuu na pia urahisi wa kuweka na kutoa fedha. Kadi hii pia italindwa kwa neno la siri (PIN) na teknolojia ya juu ya ulinzi. Kwa maana hiyo watumiaji wa kadi ya Mimosa wanaweza kutoa fedha katika mashine za kutolea fedha (ATM), kufanya malipo ya kutumia kadi katika maeneo yote yenye huduma hiyo na pia kufanya manunuzi mtandaoni mahali popote duniani kupitia mtandao wa Visa.  Vile vile wateja wanaweza kuweka pesa katika kadi zao kupitia tawi lolote la UBA Tanzania au mitandao ya simu M-pesa, Tigo Pesa, Airtel Money na pia katika akaunti za kukusanya fedha katika benki za CRDB na Exim.
“Tanzania tayari ina mfumo wa teknolojia ya kuwa jamii isiyotumia fedha. Kupitia kadi zetu tunawahamasisha wateja wetu kupokea mfumo huu wa kufanya malipo bila kutumia fedha. Zaidi ya hapo wateja wetu watapata punguzo la bei katika baishara mbalimbali sio tu Tanzania bali barani Afrika na baadaye ulimwengu mzima watakapofanya manunuzi kupitia kadi hizo. Wateja pia wanaweza kupata fedha za dharura hadi shillingi Milioni moja kwa riba ya asilimia sifuri,” aliongeza Raymond.
Naye Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha za Kielektroniki wa UBA Tanzania, Tesha Philemon, alisema kuwa “ Lengo letu kuu ni kubadilisha mfumo wa jinsi watu wanavyotumia huduma za kibenki haswa kwa kujikita katika kundi la wale ambao hawatumii huduma za benki kwa kupitia teknolojia kama hizi. Tunaamini kuwa ushirikiano huu kati ya UBA Tanzania na Regency Innovation Solutions utafanikisha lengo letu la kuwafikia wale wasiotumia huduma za benki na kuwajumuisha katika huduma hizi katika Tanzania na bara la Afrika.
Tanzania ni nchi ya kwanza katika ushirika huu kuanza kutumia teknolojia hii. Kampuni ya Regency Innovation Solutions tayari ina miradi kama hii katika nchi za Zambia na Uganda na wana mpango mkubwa wa kuleta mabadiliko makubwa katika kutoa vitambulisho kwa kutoa vitambulisho vya ushirika vya Visa kwa wanafunzi na makampuni na katika siku za karibuni pia watazindua kadi za malipo kabla za Visa za Dhahabu na Platinum.
Fursa
  • Kuwa wakala wa usambazaji wa kadi hizi tafadhali tuma barua pepe kwa Meneja wa Akaunti kupitia : RegencyInnovation@gmail.com
  • Kusajili kampuni yako kuwa katika orodha ya biashara zitakazotoa punguzo kwa wateja zaidi ya 500 wa kadi za Mimosa, tutumie barua pepe kwa Meneja wa Akaunti kupitia : RegencyInnovation@gmail.com

0 maoni:

Chapisha Maoni