Jumamosi, 21 Mei 2016

DC. BAGAMOYO AKABIDHI MADAWATI 50 KWA SHULE MBILI ZA MSINGI


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Hemed Mwanga,kulia mwenye miwani. akimkabidhi mwalimu mkuu wa shule ya msingi Majengo madawati.


Na Athumani Shomari, Bagamoyo.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid HEmedi Mwanga amekabidhi madawati 50 kwa shule mbili za msingi ikiwa ni mkakati wa mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Everisti Ndikilo wa kuondoa uhaba wa madawati unaozikabili shule za mkoa wa Pwani.

Madawati hayo 50 yenye thamani ya shilingi milioni nne yamekabidhiwa kwa shule za msingi Majengo na Mbaruku zote za Bagamoyo mjini.

Majidi amewashukuru wadau wa maendeleo ya elimu wilayani Bagamoyo ikiwemo kampuni ya Kirai Pateli ambayo ndiyo imetoa madawati hayo 50 ili kuondoa tatizo hilo kwa shule za serikali huku Shubashi Pateli amtoa ahadi ya kutengeneza madawati yote yanayohitajika kwa shule za Bagamoyo ambayo ni 1,353. 

Ili kwenda sambamba na agizo la mkuu wa mkoa wa Pwani ambae amesema mpaka kufikia tarehe 30 may shule zote za mkoa wa Pwani ziondokane na uhaba wa madawati.

Aidha, amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo ya elimu wilayani Bagamoyo kuendelea kuchangia mahitaji mbalimbali ya elimu katika wilaya ya Bagamoyo na kuongeza kuwa mara baada ya kukamilisha madawati yanayhitajika kwa shule zote wilaya imepanga kuanza kazi ya umaliziaji wa maabara za shule hivyo michango inahitajika kutoka kwa wadau mbalimbali ili kufikia malengo.

Kati ya madawati hayo 50 ishirini na manane yamekabidhiwa kwa shule ya msingi Majengo huku Ishirini na mawili kukabidhiwa kwa shule ya msingi Mbaruku na kumaliza tatizo la madawati kwa shule hiyo ya Mbaruku.

Awali akiongea mbele ya mkuu wa wilaya mkuu wa shule ya msingi Majengo Andulile Lukama amesema shule ya Majengo ina madawati 250 na ina upungufu wa madawati 109 na kwamba inakabiliwa pia na upungufu wa vyumba vya kusomea hali inayopelekea wanafunzi kuingia kwa zamu ambapo darasa la nne na la sita wanalazimika kutoka saa saba ili kuwapisha darasa la tano na la tatu.

Aidha, mwalimu mkuu huyo wa shule ya msingi Majengo Andulile Lukama na mwalimu mkuu wa shule ya msingi Anna Kisonso wamemshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa juhudi ya kutafuta wahisani ili kusaidia kuondoa changamoto zinazozikabili shule za serikali wilayani hapa.

Wakati huohuo Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Hemed Mwanga, amewataka walimu wakuu wa shule zote za Bagamoyo kuacha tabia ya kutumia madawati ya shule kwa shughuli za mikutano ya hadahara.

Majid amesema kuwa madawati ni kwaajili ya wanafunzi kusomea hivyo ni marufuku kuytatumia kwaajili mikutano ambayo haihusiani na shule.

Amesema kitendo cha kutoa madawati nje kwaajili ya mikuatano mbalimbali kinachangia uharibifu wa madawati hayo na baadae kupelekea usumbufu kwa wanafunzi.

0 maoni:

Chapisha Maoni